• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Dkt Gwajima ampa siku 30 Katibu Tawala Mkoa Pwani kufanya tathmini ya kina kwenye Mradi wa Tumbi Hospitali.

Posted on: March 4th, 2021

 Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Dkt  Dorothy Gwajima ametoa siku 30 kwa Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Dkt  Delphine Magere kusimamia kamati inayofuatilia mradi wa upanuzi uboreshaji wa hospitali ya Rufaa ya Tumbi iliyopo Kibaha Mkoani Pwani ambao.umekwama kwa miaka kumi sasa.

Dkt Gwajima alitoa agizo hilo Machi 4,2021 Mjini Kibaha alipofika kufuatilia utekelezaji wa maagizo yake aliyoyoyatoa Desemba 24, 2020 alipotembelea katika Hospitali ya Tumbi kukagua huduma zinazotolewa pamoja na upanuzi wa majengo ya  mradi huo.

Miezi miwili iliyopita Waziri huyo alitoa maagizo kwa Katibu Tawala wa Mkoa huo baada ya kubaini mradi huo kukwama utekelezaji wake kwa muda mrefu huku fedha zilizotajwa awali zikiongezeka kutoka Bilion tano hadi 29.

" Leo nimepokea taarifa ya Katibu Tawala niliyomuelekeza kufuatilia na kufanya tathmini katika uboreshaji na upanuzi wa majengo haya ya Hospitali hii ya  Tumbi, sasa natoa tena siku 30 ifanyike tathmini ya kina kwenye mradi huo baada ya hii ya awali kuonyesha mapungufu na hasara " alisema Dkt Gwajima.

Aidha alisema kuwa  katika ripoti aliyokabidhiwa na Katibu Tawala ilionyesha upotevu wa Shilingi Bilion 1.6 pia mkanganyiko wa wakandarasi wawili katika mradi huo ambao ni Suma JKT na Must Construction bureau.

"Ifanyike tathmini ya kina kwa mradi mzima siku zisizozidi 30 rejeeni katika vipimo vya jengo zima, kamati pia ihakiki uhalali wa Shilingi Bilion 29 wakirejea mpango wa upanuzi wa majengo zibainishwe sababu za ongezeko za fedha hizo kutoka Shilingi abilion 5" alisisitiza.

Gwajima alisema katika taarifa ya upanuzi wa majengo hayo makadirio yaliyofanywa na Mkoa yalilenga kutumia Shilingi Bilion tano kabla ya Serikali kuonyesha nia ya kufanya upanuzi katika mradi huo ambapo mapendekezo yalielezwa kuwa ni Shilingi Bilion 29 badala ya ile ya awali kwa majengo hayo.

Nae Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Dkt  Delphine Magere alisema amekabidhi ripoti hiyo ambayo imeeleza namna fedha zilizotolewa na Serikali zilivyotumika na upotevu uliobainika.

Dkt Magere alisema Serikali na wadau wamechangia kiasi cha Shilingi Bilion 9.4 kwa ajili ya upanuzi wa majengo hayo na kwamba hadi sasa Shilingi Bilion 5.5 zimetumika.

Alisema katika fedha hizo zilizotumika hakuna uhalisia wa thamani ya fedha, na kwamba upotevu uliobainika ni upande wa sampuli ya vipimo na si mradi mzima.

" Ripoti ya awali tuliyoikabidhi imeonyesha malipo hewa ambayo hayakufuata taratibu, sasa tunakwenda kufanya tathmini kugusa mradi mzima na ripoti yetu itaonyesha uhalisia wa hasara iliyobainika, kwa siku 30 tulizopewa tutaweza kukamilisha kwani mapungufu mengi tumeahayabaini tutakamilisha kwa wakati" alisema Dkt Magere.

Mganga mkuu wa Mkoa wa Pwani Dkt  Gunini Kamba alisema pamoja na kuchelewa kukamilika mradi huo lakini ulazima wa upanuzi bado upo.

Gunini alisema michoro ya awali ilishapitwa na wakati na kwamba itachorwa mipya na kwamba maboresho na upanuzi utakapokamilika huduma za kisasa zaidi zitatolewa katika Hospitali hiyo.

Msanifu wa Majengo  wa Mkoa wa Pweani Paul Korosso alikiri kuwepo na mkanganyiko wa wakandarasi wawili katika mradi huo na kwamba jambo hilo litabainika zaidi katika tathmini itakayofanywa kwa siku siku 30.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.