• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Awamu ya Kwanza Ujenzi Kongozi KAMAKA kukamilika Februari

Posted on: January 9th, 2024

Awamu ya kwanza ya ujenzi wa miundombinu ya Kongani ya kisasa ya viwanda "Modern Industrial Park" iliyopo Disunyara, Mlandizi Kibaha mkoani Pwani (KAMAKA) imefikia asilimia 93 ya utekelezaji.

Mradi huo unaotarajia kugharimu shilingi trilioni 3.5 hadi kukamilika, unatarajia kukamilisha awamu hiyo ya kwanza Februari 2024.

Hayo yamebainika katika ziara ya Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji aliyetembelea kongani hiyo ili kujionea maendeleo ya hatua za utekelezaji na changamoto zilizopo ili kuzibeba na kwenda kuzifanyia kazi kupitia mawaziri wa kisekta.

Taarifa za utekelezaji zimeeleza kuwa katika kiasi hicho cha shilingi trilioni 3.5, bilioni 122.4 zitajenga miundombinu ndani ya kipindi cha miaka mitano ambapo hadi sasa sh. bilioni 35 zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu hiyo na gharama zinazohusiana na uwekezaji huo.

Aidha Kijaji amesema ujenzi wa viwanda na kongani za kutosha nchini utawezesha kupunguza changamoto ya ajira kwa vijana wa kitanzania.

Akizungumzia changamoto za kongani hiyo, Kijaji amesema zipo ambazo zimeanza kufanyiwa kazi na akaahidi kukaa na waziri wa ujenzi Innocent Bashungwa ili kuangalia namna ya kufanikisha ombi la ujenzi wa barabara iendayo kwenye Kongani hiyo.

Aidha, Waziri Kijaji amempongeza mwekezaji huyo wa ndani KAMAKA Co.Ltd kwa kuthubutu na kuwa na uthubutu wa uwekezaji huo mkubwa.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge ameeleza kuwa barabara ya kuanzia Makofia -Mlandizi -Mzenga -Vikumburu -Mloka ni muhimu kwani inapitia eneo la uwekezaji na lenye miradi ya kimkakati.

Kunenge ameomba kuwa wakati ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami ukianza, uanzie Mlandizi kwa maslahi mapana ya eneo hilo.

Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa kuhusu changamoto ya maji, alishaongea na waziri wa maji Jumaa Aweso ambae aliahidi kufika kwenye kongani hiyo kujionea uhalisia wa tatizo.

Akisoma taarifa ya mradi huo Mkurugenzi wa Afriq Engineering and Construction Campany Liited Mhndisi Charles Bilinga alisema makadirio  ya awali yamaonesha kuwa  ajira zisizopungua 200,00 zitatokan na mradi huo ulioanza oktaba 2021 kwa wakazi wa maeneo ya jirani na Kongani ambapo ajira za moja kawa moja zinakadiriwa kuwa 30,000 na pato la serikali litaongezeka kupitia kodi mabalimbali

Mhandisi bilinga alisema gharama za mradi huo hadi kukamilika ni Trilion 3.5 .

Nae  afisa Fedha na Masoko  wa Turnkey Real Estate, Tumaini Kabengula, ameeleza kuwa mpaka sasa kuna mikataba 1o ya ununuzi wa Viwanja kwa ajili ya ujenzi wa viwanda , Kuna viwanja 24 vilivyoshikiriwa vikisubiri kusainiwa  kwa mkataba , wawekezaji watatu wamekwishaanza hatua za awali za ujenzi na wengine watano waliosani mikataba wataanza mwaka huu.

Alisema  wawekezaji waliotembelea kongani kwa nia ya kuwekeza ni 58 wakitokea nchi za India, China ,Uturuki ,Sudan ya Kusini . Afrika ya Kusini ,Rwanda ,Somali, Pakistan,Yemen, Falme za Kiarabu,Misri, Canada ,Uganda, Kenya na Tanzania.

"Mradi ulianza kutekelezwa oktoba 2021 kwa awamu ya kwanza kwenye ujenzi wa lango kuu na uzio, kituo cha Polisi, jengo la Utawala, Ofisi na jengo la makazi ya wafanyakazi wa Zimamoto, Zahanati, kituo cha Umeme wa megawatt 54 , mfumo wa barabara za nje na ndani na umefikia asilimia 93," alibainisha Mhandisi Bilinga

.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.