• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Dkt . Mpango atoa maagizo kwa Wakuu wa Mkoa wote

Posted on: August 22nd, 2023

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. philip Mpango ametoa maagizo saba kwa wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala Tanzania bara yatakayowaongoza kusimamia na kutekeleza ipasavyo majukumu kuwahudumia wananchi katika maeneo yao.

Dkt. Mpango ametoa maagizo hayo leo Agosti 22, 2023 wakati akifungua mafunzo ya siku sita ya Uongozi kwa viongozi hao katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Kibaha kwamfipa mkoani Pwani.

Miongoni mwa maelekezo aliyoyatoa ni pamoja na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa kuzingatia maadili na nidhamu ya Utumishi wa Umma katika maeneo ya kazi, ushirikishwaji na utatuzi wa kero zinazowakabili wananchi na kutoa mapendekezo juu ya mambo mbalimbali ambayo yanapaswa kurekebishwa na serikali.

“Jambo lingine la muhimu sana ni dhana ya usiri, kipindi hiki cha utandawazi ni muhimu kuwa makini na wasiri wa mambo ya serikali, tuzingatie hilo kwa ajili ya ulinzi na usalama wa nchi yetu na kuhakikisha tunaongeza umakini katika usimamizi wa rasilimali za umma na kutekeleza kikamilifu miradi ya maendeleo," amesema Dkt. Mpango.

Aidha amewataka viongozi hao kutoa elimu kwa watendaji wao kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi sambamba na kutangaza fursa zitokanazo na uhifadhi, ikiwa ni pamoja na biashara ya hewa ya karbon na uchumi wa bluu.

“Jitahidini kuziwezesha sekta binafsi kwa kuweka mazingira yenye vivutio ili wawekezaji kama washirika muhimu kwenye suala zima la maendeleo waje kwa wingi kwenye maeneo yenu badala ya kuwahitaji kwenye uchangiaji wa shughuli zenu kama vile mwenge,” ameongeza Dkt Mpango.

Amesema, mafunzo hayo yatawasaidia viongozi hao kusimamia matumizi ya fedha, lakini pia kuwawezesha kuratibu upandishaji wa vyeo vya watumishi bila upendeleo na vile vile kujibu barua mbali mbali za wanachi na za viongozi kwa wakati.

Amewaeleza viongozi hao kushughulikia mapema changamoto zozote zinazojitokeza kwenye jamii na akawaasa kujitahidi kusoma na kuelewa ipasavyo nyaraka mbali mbali za Serikali, kama vile Ilani ya Chama cha Mapinduzi - CCM, Mpango Mkakati wa Maendeleo wa 2020/2025 pamoja na sheria mbali mbali za nchi huku akiwafahamisha kuwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua uwepo wa viongozi hao kwenye mafunzo hayo na kuwa ndiye aliyetoa muongozo ili yafanyike.

Awali, akitolea ufafanuzi juu ya umuhimu wa mafunzo hayo kwa Wakuu wa Mikoa na makatibu Tawala wa Mikoa, Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI Angela Kairuki amesema yatasaidia kuongeza ubunifu na weledi katika kutekeleza majukumu yao.

Amesema jumla ya mada 20 ambazo zimesheheni masuala mbalimbali ya utumishi wa umma zitafundishwa na kwamba wakimaliza mafunzo hayo watakuwa na ujuzi na maarifa ya kutosha.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge ambaye ni mwenyeji wa viongozi hao katika Mkoa huo anashiriki kikamilifu mafunzo hayo kwa ajili ya kumuwezesha kusimamia kikamilifu majukumu yake na kuufanya mkoa wa Pwani kuendelea kuwa kinara wa uwekezaji katika sekta ya viwanda, biashara, kilimo na uvuvi.

Mafunzo kwa viongozi hao yatahitimishwa Agosti 27, 2023.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.