Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, Mhe. KanaliJoseph Kolombo, leo amezindua rasmi mnada wa kwanza wa zao la ufuta kwa msimuwa mwaka 2025, uliofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti, mkoaniPwani.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Juni 12Wilayani Kibiti, Kanali Kolombo amewatakawakulima kuzingatia taratibu na kanuni za kiserikali katika uuzaji wa mazaoyao, huku akisisitiza umuhimu wa kupeleka mazao kwenye maghala rasmi kama hatuaya kulinda maslahi ya mkulima na Halmashauri.
“Katika kipindi hiki chamavuno, baadhi ya watu wamekuwa wakihangaika kuuza mazao bila kufuatautaratibu. Utoroshaji wa mazao siyo tu ni kinyume cha sheria, bali piaunalinyima eneo husika mapato halali na kudhoofisha takwimu za maendeleo zaWilaya na Mkoa,” amesema Kanali Kolombo.
Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya amezielekeza taasisi za fedhakuhakikisha zinatoa huduma kwa weledi ili kuwawezesha wakulima kufungua nakutumia akaunti kwa urahisi, jambo litakalosaidia kuimarisha mzunguko wa fedhavijijini. Pia amewataka wanunuzi wa mazao kuhakikisha wanalipa fedha zawakulima kwa wakati ili kuwawezesha kufidia gharama za uzalishaji.
Katika mnada huo wa kwanza, bei ya kilo moja ya ufuta ilifikiaShilingi 2,414.49. Mnada mwingine unatarajiwa kufanyika tarehe 19 Juni, 2025katika eneo la Kingoma AMCOS, Wilaya ya Mkuranga.
Mnada huu unatajwa kuwa hatua muhimu katika kuinua uchumi wawakulima wa Mkoa wa Pwani kupitia uuzaji wa mazao kwa mfumo rasmi unaolindahaki na mapato ya pande zote.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
Sanduku la Posta: 30080 Kibaha
Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500
Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500
Barua pepe: barua@pwani.go.tz
Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.