• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Kataraiya azindua Mafunzo ya Ujenzi kwa mama Vijana

Posted on: January 14th, 2025


Katibu Tawala Msaidizi wa Idara ya Mipango, Bibi Edina Kataraiya, amezindua kikao cha kuratibu mafunzo kupitia Mradi wa Mwanamke na Ujuzi kwa Mama Vijana. Mradi huu unasimamiwa na Taasisi ya Anjita kwa kushirikiana na Serikali ya Mkoa wa Pwani.

Kikao hicho, kilichofanyika leo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, kimehusisha wanafunzi wa mafunzo hayo, Taasisi ya TAWAH inayotoa mafunzo, Shirika la Swiss Contact kama wafadhili wa mradi, wazazi wa wanafunzi, na baadhi ya watumishi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Mradi huu unalenga kuwapa ujuzi mama vijana 16 (waliozaa wakiwa na umri mdogo) katika fani ya ujenzi. Mafunzo hayo, yatakayoanza rasmi tarehe 20 Januari 2025, yatafanyika katika Chuo cha Mafunzo ya Ujenzi kilichopo Kijiji cha Muhaga, Wilaya ya Kisarawe, Mkoani Pwani.

Mafunzo hayo yatajumuisha hatua mbalimbali za ujenzi, kama vile Kuchanganya udongo na saruji, Kutafsiri michoro ya ujenzi, Kutengeneza matofali, Kupaua na kupaka rangi, Kuweka umeme katika nyumba, Kuchimba msingi, kuchanganya zege, na kujenga nyumba hadi kukamilika.

Akizungumza kwenye kikao hicho, Bibi Edina aliwasihi wanafunzi kusoma kwa bidii na kuwa na nidhamu, akibainisha kuwa mafunzo hayo ni fursa muhimu kwa maisha yao. Alisema:

“Mjione wenye bahati kwa kuwa masomo haya yanatolewa bure. Niwasihi msome kwa bidii, muwe na nidhamu, na tabia njema. Hii itawasaidia kujitegemea kiuchumi na kupata fursa zaidi kutoka kwa wafadhili.”

Aidha, aliwahamasisha kuwa mafunzo hayo ni suluhisho kwa changamoto zinazowakumba mama vijana. Aliongeza:

“Kuzalishwa siyo mwisho wa maisha. Kupitia mafunzo haya, tutapata ujuzi utakaotuwezesha kuanzisha biashara zetu na hata makampuni ya ujenzi.”

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Mwanamke na Ujuzi kutoka Swiss Contact, Bwana Helmani Nishani, alisisitiza kuwa mafunzo hayo yatatolewa bure bila gharama yoyote kwa wanafunzi.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Anjita, Bibi Janeth Mlale, alieleza kuwa taasisi hiyo kwa sasa ina zaidi ya wanafunzi 300 wanaoendelea na mafunzo katika fani mbalimbali, kama vile ushonaji, saluni, ufugaji, kilimo, uchakataji samaki, na uzalishaji wa mwani, katika Wilaya za Bagamoyo na Kibaha, Mkoani Pwani.

Mradi huu unatarajiwa kubadilisha maisha ya mama vijana kwa kuwapa ujuzi wa kujitegemea na kuchangia maendeleo ya jamii nzima.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.