• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa uhuru awataka Wanzania kudumisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Posted on: April 5th, 2025

Kiongozi wa Mbio za Mwenge awataka Watanzania kudumisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

 Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Ismail Ussi, amewataka Watanzania kudumisha amani na utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Hayo ameyanzungumza  leo Aprili 5 wakati alipokuwa akiendesha mbio hizo katika Wilaya ya Rufiji, mkoani Pwani, Ussi aliwasihi wananchi kushiriki uchaguzi kwa njia ya amani na kuzingatia ujumbe wa Mwenge wa mwaka huu unaosema: “Jitokeze kushiriki Uchaguzi Mkuu 2025 kwa amani na utulivu.”

Mwenge wa Uhuru ulikagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo, pamoja na kuwasilisha ujumbe wa kitaifa wa Mbio za Mwenge kwa wananchi wa Rufiji.

Ussi alisema ameridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo aliyokagua, na akawataka viongozi na wananchi kuhakikisha fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya miradi hiyo zinatumika kwa ufanisi na uadilifu.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Rufiji ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, alisema Mbio za Mwenge zimeendelea kuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo kutokana na kufika kila pembe ya nchi.

Mchengerwa alieleza kuwa serikali itaendelea kupokea na kufanyia kazi maelekezo yanayotolewa na viongozi wa Mbio za Mwenge, sambamba na kuhakikisha wananchi wote wanashiriki kikamilifu katika maeneo yote ambayo mwenge unapita.

Aidha, aliipongeza Serikali kwa kuidhinisha fedha za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo, hatua ambayo amesema imechochea kasi ya maendeleo ikilinganishwa na hali ya miaka 60 iliyopita.

“Katika kipindi cha hivi karibuni, Rufiji imepiga hatua kubwa katika sekta ya miundombinu, ujenzi wa shule na vituo vya afya. Shule zaidi ya 10 zimejengwa, na vituo vya afya vimeongezeka kutoka viwili hadi kufikia tisa,” alisema Mchengerwa.

Mwenge wa Uhuru umepitia jumla ya miradi sita ya maendeleo wilayani Rufiji, yenye thamani ya shilingi bilioni 1.6. Miongoni mwa miradi hiyo ni uzinduzi wa bweni katika Shule ya Sekondari ya Ikwiriri lenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 80.



Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.