• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Kiwango cha Maambukizi ya VVU chashuka Pwani-RC Ndikilo

Posted on: October 19th, 2018

Kiwango cha Maambukizi ya Ugonjwa wa UKIMWI Mkoani Pwani kimeshuka kutoka asilimia 7.1kwa mwaka 2003 hadi  asilimia 5.5  Mwaka 2017.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mh.  Mhandisi Evarist Ndikilo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kupima VVU na kuanza dawa mapema kwa wenye maambukizi Mkoa wa Pwani.

Ndikilo alisema kuwa katika kipindi hicho maambukizi  yameshuka  kutokana na mafanikio mazuri ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI Mkoani Pwani na  nchini kwa Ujumla

"Kampeni hii ambayo imepewa jina la Furaha yangu – Pima, Jitambue - Ishi inatoa ujumbe wa furaha kwa wote wanaopima na kujua hali zao za maambukizi na kwa wale wanaokutwa nayo wanaanzishiwa matibabu tofauti na zamani mpaka kinga za mwili (CD4) zishuke," alisema Mhandisi  Ndikilo.

Aidha alisema kuwa Tanzania ni kati ya nchi zinazoonyesha mafanikio katika   mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU  kwa kiwango kikubwa.

"Tanzania imekuwa kati ya nchi zinazoonyesha mafanikio katika kupambana na maambukizi ya VVU kwa kiwango kikubwa.Takwimu za utafiti wa viashiria vya VVU na UKIMWI nchini kwa mwaka 2016-2017 unaonyesha  kushuka kiwango cha maambukizi kutoka asilimia 7 mwaka 2003 hadi   asilimia 4.7,"alisema Ndikilo.

 

Pia alisema kuwa hali ya kutojua hali zao za maambukizi ya VVU huleta athari kubwa kwa wenza na familia zao na inadhoofisha mapambano kwa Mkoa na nchi nzima kwa ujumla na zaidi kufikia malengo ya Millenia ya kupambana na ukimwi ya mwaka 2020 na 2030.

Mhandisi Ndikilo aliwataka watu  wajitokeze kwa wingi kupima VVU ili kujua hali zao na wale wanaogundulika waanze dawa mapema na wasikubali kudanganyika kuacha dawa hizo mara afya zao zinapoonekana kuimarika.

Naye kaimu mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Dk.Hussein Athuman alisema kuwa takwimu zinaonyesha kuwa jumla ya watu 307,486 sawa na asilimia 87 wamepatiwa huduma ya upimaji VVU kwa kipindi cha Januari hadi Septemba 2018.

Dk Athuman alisema idadi hiyo ni tofauti na mwaka 2017 waliopima walikuwa watu 189,005 kwa kipindi kama hicho.

Alisema kuwa changamoto waliyonayo ni kukosekana kwa mashine ya kupima wingi wa VVU na kulazimisha kutuma sampuli hospitali ya Lugalo hivyo kuchelewesha majibu na upungufu usioridhisha wa virusi katika kundi la watoto chini ya miaka 15 kutokana na ufuasi usioridhisha wa matumizi ya dawa.

" Huduma hizi zimefanyika kwa kushirikiana na Thps ambao wameimarisha huduma za upimaji katika Hospitali,vituo vya afya na zahanati kwenye mkoa wetu,"alisema Dk Athuman

Wadau ambao wameshiriki kwenye mapambano hayo ni Serikali ya Marekani kupitia mradi wa PEPFAR,mfuko wa dunia kupambana na Ukimwi,kifua kikuu na Malaria,asasi za kiraia za mapambano dhidi ya ukimwi THPS,ICAP,UMB,Pact-Kizazi kipya,Jsi,viongozi wa dini na vyama vya siasa.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.