• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Kunenge alitaka Baraza Pwani kukuza Biashara

Posted on: May 13th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge, amelitaka Baraza la Biashara Mkoni humo kuandaa Mikakati Madhubuti ya Kukuza biashara na kuvutia wawekezaji katika kufursa mbalimbali zilizopo mkoani humo.

Kunenge ameyasema hayo leo Mei 13, 2024, wakati akifungua Mafunzo ya siku mbili ya uendeshaji na Majadiliano kati ya Sekta ya Umma na Binafsi katika Mkoa wa Pwani, yanayoratibiwa na Idara ya Uwezeshaji Kiuchumi na Maendeleo ya Sekta Binafsi, kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu.

Amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa ya kutafuta wawekezaji kuja kuwekeza hapa nchini ambapo Mkoa wa Pwani ni miongoni mwa Mikoa inayonufaika na jitihada hizo na kuwa ni wa kwanza kwa uwingi wa Viwanda nchini, hivyo akalitaka Baraza hilo kuunga mkono jitihada hizo kwa kuhakikisha mazingira ya Uwekezaji Mkoani Pwani yanaboreshwa.

“Ndugu zangu wana Pwani Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa na maono na miongozo mizuri ya namna ya kuliongoza vyema Taifa hili na kukuza uchumi wake kupitia sekta mbalimbali ikiwemo Viwanda, Biashara na Uwekezaji," amesema.

Ameliambia Baraza hilo kuwa linatakiwa kuzingatia vipaumbele vya Rais katika kukuza uchumi na kuongeza wawekezaji hapa nchini kwa kuwezesha mazingira mazuri ya biashara na uwekezaji.

“Mkoa wa Pwani, umejaaliwa kuwa na fursa za kipekee za kijiografia na rasilimali nyingi ambazo tukiweza kuzitumia vizuri kupitia mashirikiano ya Sekta Binafsi na Sekta ya Umma tutaweza kupiga hatua kubwa katika maendeleo ya kiuchumi," amesema.

“kwa muda mrefu Mkoa wa Pwani umekuwa mdau muhimu katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa Tanzania kupitia fursa za kijiografia na miundombinu wezeshi ikiwemo barabara, reli, umeme na maji. Fursa hizo zimeufanya Mkoa huu kuwa rahisi kufikika.” amebainisha Kunenge na akasema kuwa Mafunzo hayo yaende sambamba na majadiliano ya kimkakati ya kukuza ufanisi kwenye viwanda ili kutoa mchango wa Mkoa katika pato la Taifa.

Mkuu huyo wa Mkoa pia amezielekeza Taasisi wezeshi kuweka mazingira rafiki miundombinu yote muhimu inakuwepo, akitolea mfano Miondombinu ya Barabara, maji na Umeme ili kuendelea kuvutia uwekezaji mwingi katika mkoa huo huku akitahadharisha kuwa hayupo tayari kusikia kuna uwekezaji umeingia mkoani humo ukafa ama kufungwa na kuhamishwa kwenda nje ya eneo hilo akisema “ni mkakati gani ambao tunao kama Baraza la biashara la mkoa ili tujue kuwa sisi kama mkoa tunataka kwenda wapi," amesisitiza Kunenge.

Kwa Upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Uwezeshaji Kiuchumi na Maendeleo ya Sekta Binafsi Kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Bw. Conrad Milinga, Ameeleza kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuyajengea uwezo mabaraza ya biashara na kuwaleta pamoja wadau wa sekta binafsi na sekta ya umma ili kufanya kazi kwa Pamoja kama wabia.

Milinga amesema mabaraza hayo pia yanatakiwa kutambua kwamba sekta binafsi ndio inaendesha uchumi, kuongeza ajira na kuchakata na kuongeza thamani ya mazao yanayozalishwa ndani ya nchi ili kuweza kuongeza mapato ya Serikali. na kuwa sekta hizo kwa pamoja ni wadau wakuu wa serikali hivyo ni lazima watambuane na kushirikiana.

Amesema kumekuwa na pengo kubwa kati ya ushirikiano wa kimajukumu kati ya sekta binafsi na za umma jambo hilo sasa linakwenda kuondolewa kupitia majadiliano ambapo kila mmoja atapata nafasi ya kuzungumza na kueleza changamoto zilizopo na namna ya kuzitatua.

Akitoa mada kwenye mafunzo hayo, Afisa Mkuu wa Uchumi, biashara na uwekezaji Mwamini Nkwizu amesema mabaraza ya biashara nchini yamefanya kazi kubwa kuongeza na kuchochea tija katika masuala mengi ambayo yalikuwa na ukinzani japo pia aliyataka kutengeneza ajenda za pamoja kama mkakati wa kuondokana na changamoto zilizopo.

Amesema maeneo mengi yaliyofanyiwa utafiti na tathmini iliyotolewa na ofisi ya taifa ya Takwimu NBS inaonesha kuwa mkoa wa Pwani umefanya vizuri katika kusimamia mabaraza hayo kwa kushika nafasi ya pili hususani pia katika kuweka manegementi nzuri kwa kuwasiamia wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama "machinga."


Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.