• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Kunenge Aomba Timu Kusimamia Urereshaji wa Huduma ya Vivuko Mafia

Posted on: October 26th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, ameomba kuundwa kwa timu maalum ili kusimamia urejeshaji wa huduma ya vivuko vya MV Kilindoni na Meli ya TSN Songosongo vinavyotoa huduma ya usafiri kati ya Nyamisati, Wilaya ya Rufiji, na Mafia, baada ya huduma hiyo kusimama tangu Oktoba 10 mwaka huu. Kunenge alitoa ombi hilo leo akiwa katika ziara ya ukaguzi na uzinduzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Mafia, akiwa ameambatana na Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa.

Kunenge alitoa wito huo katika ofisi ya Wilaya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Mafia, akiomba timu ya watu watakaosimamia urejeshaji wa huduma hizo muhimu.

Baada ya kupokea ombi hilo, Waziri Bashungwa, akiwa katika ukaguzi wa matengenezo ya Meli ya TSN Songosongo yanayosimamiwa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kupitia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, aliagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi kuunda timu itakayojumuisha Ofisi ya RAS Pwani, Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Uchukuzi, TEMESA, JWTZ, na wadau wengine ili kutafuta suluhisho la kudumu kwa changamoto ya vivuko wilayani Mafia.

Hatua hii imechukuliwa baada ya vivuko vya MV Kilindoni na Meli ya TSN Songosongo kuharibika, hali iliyosababisha kukwama kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi wilayani humo.

Bashungwa alieleza kuwa serikali inatambua umuhimu wa huduma za usafiri wa vivuko katika Wilaya ya Mafia, na imechukua juhudi za kuhakikisha vivuko vyote viwili vinapatikana ili endapo kimoja kiharibike, kingine kiweze kuendelea kutoa huduma. Aliongeza kuwa serikali ina mpango wa kuongeza kivuko kingine ili kuimarisha huduma hizo.

“Serikali imechukua jitihada za haraka na makusudi, pamoja na timu hii kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, ili kurudisha huduma ya vivuko viwili,” alisema Mhe. Bashungwa.

Aidha, Waziri Bashungwa akiwa wilayani humo ameweka jiwe la msingi katika Zahanati ya Kilindoni yenye gharama ya milioni 190 kutoka Serikali Kuu, pamoja na Shule ya Sekondari ya Raphta yenye thamani ya zaidi ya milioni 500.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.