• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Maafisa Mkoa , Halmashauri za Pwani wapewa mafunzo ya mfumo wa manunuzi ya Umma(NeST(

Posted on: August 30th, 2023

Mkoa wa Pwani umeanza kutoa mafunzo ya matumizi ya mfumo mpya wa Manunuzi wa NeST kwa maafisa wa Mkoa, makatibu Tawala wa Wilaya na maafisa wa halmashauri zote za Mkoa huo nchini kwa lengo la kuutumia na kudhibiti mianya ya upotevu wa fedha pamoja na kuepukana na hoja za Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali CAG ambazo zimekuwa zikijirudia kila mwaka kuhusu upotevu wa fedha kwenye manunuzi.

Akifungua mafunzo hayo kwa maafisa washiriki leo Agosti 29,2023 kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Kaimu Tawala wa mkoa huo, Savera Salvatory, amesema mfumo huo mpya ni mbadala wa uliokuwa unatumika awali wa TANePS ambao ulikuwa na dosari nyingi ikiwa ni pamoja na kusababisha upotevu wa fedha za umma.

Amesema mfumo huo mpya umejengwa na kusimamiwa na watanzania wenyewe na kwamba utapunguza changamoto nyingi na utaondoa kazi kubwa kwa maafisa manunuzi kwa sababu mchakato wa manunuzi utaanzia kwa mtumiaji kwenye Idara au kitengo husika.

“Lengo la mfumo huu ni kuboresha na kudhibiti taratibu zote za manunuzi na kumrahisishia mtumiaji wa mfumo, ubunifu wa mfumo umetokana na kuwepo kwa changamoto mbalimbali na zingine tumezishuhudia kupitia taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG hoja zikiwa zinajirudia katika mfumo wa awali wa TANePS,” amesema Savera.

Ameongeza kuwa miongoni mwa hoja za CAG ambazo zimekuwa zikijirudia kutokana na mfumo wa TANePS ni manunuzi yasiyoingizwa katika vitabu mbalimbali, manunuzi yaliyofanyika nje ya bajeti, manunuzi yasiyo na tija kwa serikali na taratibu ndefu za manunuzi kupitia mfumo huo.

Amesisitiza kuwa mfumo huo utaanza kutumika rasmi Oktoba mosi mwaka huu ambapo taratibu zote za manunuzi zitafanywa kwa njia hiyo kuanzia uandaaji wa mahitaji ya Idara husika uanzishaji wa tenda, uthamini, utoaji wa tenda na mahojiano.

“Mfumo huu mpya umeanza kutumika Julai mosi na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi Serikalini (PPRA) na kwamba imetoa muda wa miezi mitatu hadi Oktoba mosi mwaka huu 2023 mamlaka zote kuanza kutumia mfumo wa NeST,”amefafanua Savera.

Aidha, amesema baada ya Oktoba mosi kwa yeyote atakayebainika kutotumia mfumo huo hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa Afisa Masuuli wa Taasisi ambayo haitatumia mfumo huo kupitia kifungu namba 104 (2) (d) cha sheria ya ununuzi wa umma ambacho kinatoa adhabu ya faini ya sh milioni 10 kutoka mfukoni mwa Afisa Masuuli atakayekiuka sheria hiyo.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi mkoa wa Pwani, Beda Mmbaga amesema jumla ya watumishi 104 wanapatiwa mafunzo ya matumizi ya mfumo huo mpya na kwamba elimu hiyo itatolewa mpaka ngazi ya chini ili kuhakilisha mkoa huo unaondokana na hoja za CAG kuhusu upotevu wa fedha za umma ambao unaripotiwa kila mwaka.

Amesema idadi hiyo ya watumishi 104 ni kubwa ukilinganisha na mikoa mingine na kwamba wamefanya hivyo mahsusi kwa kuwa mkoa huo ni wa kimkakati na wa viwanda hivyo watasaidia kuongeza ufanisi kwenye utendaji wa kazi zao.

Mshiriki wa mafunzo hayo Epiphanus Marcel ambaye ni Afisa Mkaguzi wa ndani Mwandamizi mkoani humo, amesema mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka kwani yatarahisisha utendaji kazi wao katika ufuatiliaji wa matumizi ya fedha na kuwa utawadhibiti baadhi ya watumishi wasiokuwa waadilifu kutumia dosari za mfumo wa awali kufuja fedha za umma.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.