• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Makamu wa Rais aipongeza Pwani kwa kusheheni Viwanda

Posted on: October 28th, 2018

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan, amesema serikali itafuatilia baadhi ya wafanyabiashara wanaodaiwa kuingiza bidhaa feki na kuuuza kwa gharama nafuu hali inayosababisha kushusha soko la ndani.

Hayo ameyasema wakati akizindua kiwanda cha African Dragon kinachotengeneza malighafi ya mabati, Zinga Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani kilichojengwa kwa thamani ya bilioni 11 na alisema kuwa suala hilo amelichukua na kuahidi kulifanyiwa kazi.

Aidha alieleza kuwa, kwa hali hiyo inakatisha tamaa na jitihada za wawekezaji wa ndani katika juhudi za serikali kuhamasisha wawekezaji kuwekeza nchini.

Mhe.Samia alielezea ,sekta ya viwanda kwa sasa ndiyo mpango wa serikali wa kihakikisha nchi inakuwa kwenye uchumi wa kati kupitia viwanda.

“Ofisi yangu imelichukua suala hilo na italishughulikia “alisisitiza Samia.

Hata hivyo aliwaasa wazazi na walezi kusimamia vijana wao kupata elimu ya ujuzi wa kuweza kuajiriwa ili kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira.

Pia aliupongeza Mkoa wa Pwani kwa kuongoza kwa kusheheni viwanda kitaifa, amewaomba kujipanga na kuvutia wawekezaji katika mkoa, kwani sio kazi rahisi.

“Katika utekelezaji wa Uchumi wa viwanda ,mtoe ushirikiano kwa wawekezaji ili kuweza kutimiza malengo ya serikali ya kuelekea uchumi wa kati “alieleza Mh.. Samia.

Akimkaribisha makamu wa Rais, Mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo alisema Mkoa huo, una jumla ya viwanda 429 ikiwemo vya kati, vikubwa na vidogo ,na kutengeneza ajira za moja kwa moja zaidi ya 20,000 na kunufaika na ushuru na kodi inazolipa viwanda hivyo.

Mhandisi Ndikilo alieleza, moja ya changamoto ni ukosefu wa soko ambapo kwa Bagamoyo tayari viwanda viwili ikiwemo cha nguzo za zege za umeme kimefungwa na kiwanda cha viungo macho kimesimamisha uzalishaji.

Alieleza umeme uliopo ni megawatts 62 mahitaji ni 79 kimkoa, wanapengo la megawatts 17 ili kupata umeme wa kutosha .

Katika hatua nyingine nae Mkurugenzi wa kiwanda hicho, Siling Soun alisema ,kilianzishwa 2015 ,kimegharimu bilioni 11 ikiwa ni gharama za mitambo na ujenzi.

Alisema, kwasasa wameshatoa ajira 50 za moja kwa moja na kulipa ushuru wa halmashauri milioni 30 mwezi june mwaka huu.

Soun alitaja changamoto zinazowakabili kuwa ni pamoja na kukatika kwa umeme na kusababisha hasara ya milioni mbili pamoja na soko kuwa sio la uhakika kutokana na uingizwaji wa bidhaa feki zinazonunuliwa na kuingizwa kutoka nje ya nchi na kuuzwa kwa gharama nafuu.

Alitaja ,changamoto nyingine ni miundombinu mibovu hali inayosababisha usafirishaji kuwa sio rafiki.

Akijibu changamoto za umeme, Naibu waziri wa nishati,Subira Mgalu alisema katika kutatua changamoto kiwandani hapo, wanatarajia kupunguza tatizo hilo kupitia ujenzi wa umeme kutoka Tegeta hadi eneo la uwekezaji (EPZA )Bagamoyo.

Alisema, kwenye masuala ya miundombinu ya umeme wameshaanza kutatua changamoto hizo kwa kuanzishwa miradi mikubwa ya umeme nchini ikiwemo stiglers gorge huko kwenye maporomoko ya mto Rufiji.

Samia yupo kwenye ziara ya kikazi ya siku sita mkoani Pwani, oktoba 24 alikuwa Bagamoyo na oktoba 25 ataendelea Bagamoyo na Chalinze ambapo oktoba 29 itamalizika.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.