• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Maonesho ya Biashara na Uwekezaji Pwani kuwa ya Kitaifa na kufanyika kila Mwaka

Posted on: December 17th, 2024

Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selemani Jafo (Mb), leo amefungua rasmi Maonesho ya Biashara na Uwekezaji yanayoendelea mkoani Pwani na kutoa agizo la kuyafanya maonesho hayo kuwa ya kitaifa kila mwaka. Mhe. Jafo amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil T. Abdallah, kuhakikisha maonesho haya yanapandishwa hadhi na kusimamiwa kwa kushirikiana na Mkoa wa Pwani.

“Sasa namuagiza Katibu Mkuu wa Viwanda na Biashara, Dkt. Hashil, kuanzia sasa maonesho haya ya viwanda, biashara, na uwekezaji yawe ya kitaifa. Yasimamiwe na Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Mkoa wa Pwani, na kila mwaka yafanyike hapa Pwani,” alisema Mhe. Jafo.

Aidha, Waziri Jafo alibainisha kuwa Mkoa wa Pwani kwa sasa ni kinara wa uwekezaji wa viwanda nchini, hivyo ni muhimu kuupa heshima kwa kuyafanya maonesho hayo kuwa ya kitaifa. Alisifu juhudi za uongozi wa Mkoa wa Pwani katika kuhakikisha mazingira rafiki kwa wawekezaji, hali inayochangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa sekta ya viwanda nchini.

Mhe. Jafo pia alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuimarisha mazingira wezeshi kwa wawekezaji. Alifafanua kuwa tangu mwaka 2021, idadi ya viwanda nchini imeongezeka kutoka viwanda 52,000 hadi zaidi ya viwanda 80,000, ikiwa ni ongezeko la viwanda 28,000. Alitoa pongezi maalum kwa Mkoa wa Pwani kwa kuchangia kwa kiasi kikubwa ongezeko hilo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, alitoa shukrani kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada za kukuza sekta ya viwanda na uwekezaji kupitia sera wezeshi. Alisema Mkoa wa Pwani umetafsiri sera hizo kwa vitendo kwa kuimarisha mazingira ya uwekezaji.

Mhe. Kunenge aliongeza kuwa serikali inaendelea kuboresha miundombinu kama vile umeme, barabara, maji, na masoko ili kuwezesha zaidi uwekezaji. Alibainisha kuwa katika sekta ya umeme, Mkoa wa Pwani umeongeza uzalishaji wa megawati 19, hatua inayochochea maendeleo ya viwanda.

Maonesho haya yanatarajiwa kuwa chachu ya kukuza biashara, uwekezaji, na uchumi wa Taifa kwa ujumla.


Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.