Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Bw. Rashid Mchatta, mnamo tarehe 4 Juni 2025, amefunga rasmi Mashindano ya Michezo ya UMISSETA ngazi ya mkoa yaliyoshirikisha Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Pwani.
Mashindano hayo yalifanyika katika viwanja vya Shirika la Elimu Kibaha, yakihusisha wanafunzi kutoka Halmashauri mbalimbali wakishindana katika michezo mbalimbali kwa lengo la kuibua vipaji na kuandaa timu ya mkoa kwa ajili ya mashindano ya kitaifa.
Katika hotuba yake ya kufunga mashindano hayo, Bw. Mchatta alikabidhi vikombe na medali kwa washindi wa michezo mbalimbali na kupongeza washiriki wote kwa kuonyesha nidhamu, ushindani wa hali ya juu na uzalendo.
Kupitia mashindano haya, timu ya Mkoa wa Pwani imepatikana na itawakilisha mkoa katika mashindano ya UMISSETA ngazi ya kitaifa yatakayofanyika mkoani Iringa kuanzia tarehe 19 hadi 30 Juni 2025.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
Sanduku la Posta: 30080 Kibaha
Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500
Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500
Barua pepe: barua@pwani.go.tz
Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.