• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Mchengerwa awataka Wakurugenzi wote kuhakikisha kuzitafutia majibu Hoja zote za CAG

Posted on: May 6th, 2024

Wakurugenzi nchini wametakiwa kuhakikisha hoja zote za mkaguzi wa hesabu za serikali CAG zitafutiwe majibu ili kuondoa hisia kuwa kuna ufisadi.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa wakati akifunga mafunzo ya siku tatu kwa Wakurugenzi wa Miji, Manispaa na Majiji yaliyofanyika kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere.

Mchengerwa amesema kuwa wanapaswa kufanya kazi kwa bidii na kusikiliza kero za wananchi ili kutekeleza dhana ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan ya kuwaletea wananchi maendeleo.

"Hapo hamkuchaguliwa kwa bahati mbaya bali ni imani aliyokuwa nayo Rais msiwe wanyonge na msishiriki vitendo vya rushwa na mnapaswa kumtanguliza Mungu kwani kuwatumikia wananchi ni ibaada,"amesema Mchengerwa.

Amewataka Wakurugenzi hao wasijikweze na wawe karibu na wananchi wajishushe wafanye kazi kwa weledi uadilifu na wasibweteke kwa kuteuliwa

"Hakikisheni mnakuwa na mahusiano mazuri na wananchi na nyie kwa nyie na watumishi na lazima wajue changamoto kwenye maeneo wanayo yasimamia na wasisubiri fedha za serikali wawashirikishe wadau na wananchi,"amesema Mchengerwa.

Amesema kuwa ukusanyaji mapato ni kipaumbele cha serikali kwani mapato yakiwa makubwa yatasaidia kutoa huduma kwa wananchi na kupeleka maendeleo kwani hilo Rais analisisitiza sana kwa maendeleo.

"Tumieni mifumo ya kieletroniki katika ukusanyaji wa mapato acheni matumizi ya fedha mbichi na kuepuka ukusanyaji wa mapato ambao hautumii mashine kwani unasababisha mapato kupotea na kuwaondoa baadhi ya watumishi wanaosababisha upotevu wa mapato na kukusanya nje ya mfumo na fedha zilizo nje zirejeshwe,"amesema Mchengerwa.

Aidha kuchukuliwa hatua kwa watumishi wasio waaminifu wasisubiri hadi waziri achukue hatua kwani wakiharibu wao ndiyo watakaowajibishwa na wawe wabunifu na wawape mafunzo maofisa biashara wasikae maofisini na waongeze vyanzo vya mapato.

Naye Annastazia Tutuba Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manyoni amesema kuwa mafunzo hayo wamewakumbusha kutekeleza majukumu yao na moja ni kukondokana na hati chafu.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Korogwe Mwashaban Mrope amesema kuwa watasimamia fedha nyingi ambazo zimetolewa na serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.