• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Mwenge wa Uhuru umemaliza mbio zake katika Halmashauri ya Chalinze

Posted on: April 10th, 2025

Mwenge wa Uhuru umekamilisha mbio zake katika Halmashauri ya Chalinze Aprili 10, 2025, ikiwa ni siku ya tisa tangu uzinduliwe katika viwanja vya Shirika la Elimu Kibaha, mkoani Pwani mnamo Aprili 2, 2025.

Katika mbio hizo, Mwenge wa Uhuru umepitia wilaya saba na halmashauri tisa, ukikagua na kuzindua jumla ya miradi 64 yenye thamani ya sh trilioni 1.028. Tarehe 11 Aprili, ambapo Mwenge huo utakabidhiwa Mkoani Morogoro.

Akiwa Halmashauri ya Chalinze Aprili 10, 2025, kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Ali Ussi, alikagua mradi wa machinjio ya kisasa ya Union Meat Abattoirs Ltd yaliyopo katika kijiji cha Kwazoka, Kata ya Vigwaza, mradi uliogharimu sh. bilioni 26.

Ussi aliwataka wafugaji kukimbilia fursa ya soko la ndani na nje kupitia machinjio hayo, akisema kuwa tofauti na miaka ya nyuma, sasa wafugaji wana uhakika wa soko kupitia uwekezaji unaofanywa ndani ya nchi.

“Haya yote ni matokeo ya jitihada pamoja na mapinduzi ya maendeleo yanayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kushirikiana na watendaji wa halmashauri, wilaya na wabunge,” alisema Ussi.

Aidha, alisifu uwekezaji mkubwa uliofanywa na Union Meat Group kwa kusogeza soko karibu na wafugaji wa ndani.

Mkurugenzi wa machinjio hayo, Mariam Mnghwani, alieleza kuwa yana uwezo wa kuchinja ng’ombe 300 kwa mstari mmoja kwa siku, pamoja na kondoo 3,000.

Pia, yana uwezo wa kuhifadhi hadi tani 150 kwa wakati mmoja na huzalisha tani tatu za nyama kwa siku, na bidhaa nyingine kama mifupa na ngozi zinazouzwa kwa wananchi.

Kwa mujibu wa Mnghwani, nyama inayozalishwa huuzwa ndani ya Tanzania na pia katika nchi za Qatar, Oman na Bahrain.

Katika siku hiyo hiyo, Ussi alizindua mradi wa maji katika vijiji vya Visezi (Chauru) na Pingo, unaotekelezwa na Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), ambao unawanufaisha wakazi 2,822 kutoka kaya 565.

Mradi huo umekamilika kwa asilimia 100 na umetumia zaidi ya shilingi milioni 206.878, sawa na asilimia 68.78 ya bajeti, chini ya mkandarasi mzawa Sajo Civil Engineering & Building Construction Ltd.

Awali akipokea Mwenge huo kutoka Kibaha, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Shaibu Ndemanga, alisema Mwenge wa Uhuru umetembelea miradi saba katika Halmashauri ya Chalinze yenye thamani ya zaidi ya sh. bilioni 28.9.

Miradi mingine iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa vyumba 50 vya biashara katika kituo cha mabasi cha Chalinze, mradi unaotekelezwa na Halmashauri hiyo kwa gharama ya shilingi milioni 216.5.

Vilevile, Mwenge umetembelea ujenzi wa shule ya Amali Msoga na mradi wa uwekaji wa taa 50 za barabarani katika kijiji cha Ruvu, Kata ya Vigwaza, uliogharimu sh.milioni 185.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.