• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Naibu Katibu Mkk OR- TAMISEMI azuru Mkoa Pwani kwa ukaguzi wa Huduma za Afya

Posted on: June 3rd, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Rashid Mchatta, leo amepokea ugeni kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI, ukiongozwa na Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya afya, Profesa Tumaini Nagu.

Ziara hiyo inalenga kufanya tathmini ya utoaji wa huduma za afya kwa wananchi, kukagua miundombinu ya afya, mifumo ya usimamizi, changamoto zinazowakabili watumishi wa sekta ya afya, pamoja na kupata mrejesho kutoka kwa wananchi kuhusu hali ya huduma zinazotolewa.

Akizungumza mara baada ya kuwasili, Prof. Nagu alisema kuwa lengo kuu la ziara hiyo ni kuhakikisha kuwa huduma za afya zinatolewa kwa ubora unaostahili na kwa kufuata miongozo ya kisera ya Serikali.

Katika siku ya kwanza ya ziara hiyo, Prof. Nagu ametembelea Halmashauri ya Chalinze, ambako alikagua Kituo cha Afya cha Chalinze pamoja na Hospitali ya Wilaya ya Chalinze iliyopo Msoga. Katika maeneo hayo, amekutana na watendaji wa sekta ya afya, watumishi wa vituo vya afya pamoja na wananchi waliokuwa wakipokea huduma, na kupata maoni yao kuhusu hali ya huduma.

Prof. Nagu anatarajiwa pia kutembelea halmashauri nyingine mbili za Mkoa wa Pwani ambazo ni Kisarawe na Rufiji, ambapo ataendelea na ukaguzi wa vituo vya afya na kuzungumza na wadau mbalimbali wa sekta ya afya.

Katibu Tawala wa Mkoa, Rashid Mchatta, amesema kuwa ugeni huo ni wa muhimu sana kwa Mkoa wa Pwani, kwani unatoa fursa ya kubaini maeneo yenye changamoto na kuweka mikakati ya kuboresha huduma kwa wananchi.

“Tunaamini kuwa kwa ushirikiano wa karibu kati ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa, tunaweza kuboresha zaidi huduma za afya na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora, kwa wakati,” alisema Mchatta.

Ziara hiyo inaakisi dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha huduma za afya kwa wananchi kupitia uwekezaji katika miundombinu, rasilimali watu, na mifumo ya usimamizi wa sekta ya afya.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Naibu Katibu Mkk OR- TAMISEMI azuru Mkoa Pwani kwa ukaguzi wa Huduma za Afya

    June 03, 2025
  • RC Kunenge aongoza kikoa cha kupitia taarifa ya Pato la Mkoa (GDP).

    June 03, 2025
  • Mkoa wa Pwani waanza maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya mtoto wa Afrika .

    May 30, 2025
  • DC Komba awahimiza Wananchi na Watumishi wa Mkoa wa Pwani Kutekeleza kwa Vitendo maono ya Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.