• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Ndikilo atilia Shaka Ujenzi wa Jengo la Ofisi za TRA Pwani

Posted on: August 28th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mh. Mhandisi Evarist Ndikilo ametilia shaka ujenzi wa jengo la Mamlaka ya mapato Tanzania  TRA Mkoa wa Pwani kwa kile alichoeleza kuwa  muonekano wa jengo hilo hauendani na thamani iliyotajwa ambayo ni shilingi bilioni  2.6.

Pia ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama Mkoa wa  Pwani kulifanyia uchunguzi suala hilo ili kuweza kubaini kama kuna ubadhilifu wowote   uliofanyika wa fedha za  Serikali.

Hayo yamebainika leo  wakati wa Ziara yake ya  ukaguzi wa majengo yaliyojengwa katika kitovu cha Halmashauri ya Mji Kibaha,ambapo alitembelea  jengo la CRDB, Jengo la Uhamiaji Mkoa pamoja na Jengo la Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Mhandisi Ndikilo alisema kuwa haridhishwi na kasi ya ujenzi  wa jengo la Mamlaka ya Mapato nchini (TRA)  ambalo ilielezwa kuwa ujenzi wake ulianza  mwaka 2015 ambapo hadi sasa bado halijakamilika huku tayari mkandarasi wa jengo hilo  ameshalipwa asilimia 61 ya fedha za ujenzi wa jengo hilo.

Akitoa taarifa ya ujenzi  wa jengo hilo kwa niaba ya Mkurugenzi , Meneja wa Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani bi Euvansia Lwiwa alisema Ujenzi wa Jengo hilo ulianza April 2015 na lilitakiwa kumalizika may 2016. Bi Euvansia alieleza kuwa  ujenzi wa jengo hilo unatarajia kugharimu  shilingi 2,693,402,120.60 pamoja na VAT  ambapo  mkandarasi wa jengo hilo Humphrey Construction ltd ameshalipwa takribani Shilingi  1,653,267,510.00 pamoja na VAT.

Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ni moja ya Tasisi ya Serikali ambayo ilipewa eneo la kujenga  Ofisi katika eneo la kitovu cha mji cha Halmashauri ya Mji Kibaha ambapo mpaka sasa ujenzi wake haujakamilika.

Katika Hatua nyingine Mhandisi Ndikilo amezipongeza taasisi za Uhamiaji, Benki ya CRDB na NMB kwa kuweza kutekeleza Agizo la  Waziri Mkuu kwa asilimia mia moja. Ikumbukwe kuwa Mhe.Waziri Mkuu alitoa agizo kwa taasisi zote zilizopewa viwanja katika kitovu cha Mji Kibaha kukamilisha ujenzi huo kwa wakati.Mhe. Waziri Mkuu alitoa agizo hilo alipokuwa akifungua jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Pwani Septemba, 2016.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.