• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Ndikilo awataka Wafanyakazi kujiepusha na Matendo ya utovu wa nidhani katika kazi.

Posted on: May 3rd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo awataka waajiri na wafanyakazi kuheshimu sheria za utumishi wa umma kwa kila mmoja kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria za nchi.

 Mhe Ndikilo ameyasema hayo katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani yaliyoadhimishwa kimkoa katika halmashauri ya Mji wa Kibaha , katika viwanja vya shirika la Elimu Kibaha na kukemea tabia za baadhi ya waajiri wasiotaka kufuata sheria za utumishi kwa kunyanyasa wafanyakazi hatakuwa tayari kufanya kazi na watu wa aina hiyo katika Mkoa wa Pwani.


Akisoma Risala ya shirikisho la wafanyakazi(TUCTA )Mkoani Pwani Bwana Ramadhani Kinyagoli aliishukuru serikali kwa jitihada zake katika shughuli za maendeleo zinazotekelezwa na serikali ya awamu ya tano kwa maslahi ya watanzania wakiwemo na wafanyakazi,hata hivyo hakusita kuwasilisha madai na changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyakazi wa Mkoa wa Pwani ikiwa ni pamoja na wafanyakazi kutopandishwa vyeo kwa wakati,kodi kubwa ya mshahara,wastaafu kutolipwa mafao yao kwa wakati,waajiri kutoheshimu sheria za utumishi kwa kutowatendea haki watumishi kwa kuwapa maslahi yao kwa mujibu wa sheria,sekta binafsi kuwazuia watumishi kujiunga na vyama vya wafanyakazi na baadhi ya halmashauri kutoitisha vikao vya mabaraza ya wafanyakazi.


Kinyangoli aliendelea kufafanua kero zinazowasibu wafanyakazi katika Mkoa wa Pwani kwa kutoa shutuma kwa baadhi ya waajiri kutotimiza ahadi zao kwa wafanyakazi hodari wa mwaka jana kwa kutowapa zawadi zao hadi sasa na kuomba Uongozi wa mkoa ulifanyie kazi kwa waajiri hao kwani ahadi zisizotekelezeka kwa wakati huvunja moyo wa utendaji kazi kwa wafanyakazi wa sekta binafsi na serikali.


Aidha Mhandisi Ndikilo aliwapongeza wafanyakazi hodari kwa mwaka 2018 kwa utendaji mzuri hata wakaweza kuteuliwa kuwa watumishi hodari kutoka katika taasisi zao .Aliendelea kulipongeza shirikisho la wafanyakazi mkoa wa Pwani kwa risala nzuri iliyosheheni mambo mazuri na yenye tija kwa mstakabari wa utumishi nchini na kusema hakika risala hii imejaa “Nondo za kutosha”Ndikilo alisema.


Pia  aliahidi kuzifanyia kazi changamoto zinazo wakabili wafanyakazi ambazo ziko ndani ya uwezo wake na kwa zile zilizo nje ya uwezo wake aliahidi kuziwasilisha kunakohusika kwa hatua zaidi. Aliwataka watumishi wa serikali na sekta binafsi kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni katika utumishi sanjari na maadili ya kazi kwa mujibu wa taaluma walizonazo.Aliwataka wafanyakazi kujiepusha na matendo ya utovu wa nidhamu katika kazi.”Lazima tuwe na nidhamu ya kazi uvivu kazini ni sumu katika ajira”Ndikilo alisema.


Mhandisi Ndikilo alisikitishwa na kitendo cha waajiri wanaotoa ahadi hewa kwa watumishi hodari na kutowatunuku zawadi zao kwa wakati hili halikubaliki hata kidogo na kutoa onyo kwa waajiri wanaobagua wananchi katika ajira hususan watu wenye ulemavu na wanawake na alisisitiza sitakuwa tayari kufanya kazi na wawekezaji wa aina hii kwani wanafanya vitu vilivyo kinyume na katiba na sheria za nchi pia.



Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.