• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Nitaendelea kuwa mkali na Mwiba kwa Mtumishi anayefanya Uzembe:DC Kawawa

Posted on: May 13th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo  Zainabu Kawawa amesema, ataendelea kuwa mkali kwa mtumishi ambaye atakuwa mzembe katika suala la ukusanyaji na udhubiti wa mapato katika Halmashauri ya Chalinze.

Kawawa aliyasema hayo juzi wakati wa kikao Maalumu Cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo kupokea taarifa ya hati ya ukaguzi wa hesabu za Halmashauri pamoja na Taarifa ya Utekelezaji wa Hoja za Ukaguzi kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

Katika kikao hicho kilichofanyika Lugoba, Kawawa alisema mtumishi ambaye hawezi kusimamisha ipasavyo mapato ya Halmashauri ni vema akaomba kuhama.

"Nitaendelea kuwa mkali na mwiba kama kuna mtu anayefanya uzembe katika suala hili tusije tukalaumiana " alisema Kawawa.

Mkuu huyo wa Wilaya pia aliwataka watumishi wa Halmashauri hiyo kuacha kulindana kwa kuwaficha wanaosababisha ukusanyaji wa mapato kuyumba na pia kuepuka kuingia mikataba na mawakala wasio waaminifu.

Alisisitiza usimamimizi katika vyanzo vya mapato ili yasishuke, huku akitoa onyo kwa wakusanyaji kuzingatia taratibu na kupeleka fedha wanazokusanya benki badala ya kukaa nazo.

Akiwasilisha maagizo kutoka kwa mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo ambaye alimwakilisha katika kikao hicho, Kawawa alisema Halmashauri hiyo imepongezwa kwa kupata hati safi kwa miaka minne mfululizo.

Alisema,Mhandisi Ndikilo pia ametoa agizo kwa Halmashauri hiyo kuepuka kuzalisha hoja kwa kuzingatia Sheria na kanuni, lakini pia ameelekeza kuimarisha kitengo Cha ukaguzi wa ndani ili kurahisisha kuibua hoja mapema na kuzifanyia kazi.

Akiongea katika kikao hicho, kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Shangwe Twamala alisema, kama kuna kesii za muda mrefu ambazo zinakuwa ngumu kuzitatua Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ishirikishwe.

Twamala alisema, Halmashauri hiyo inatakiwa kusimamia kikamilifu vikundi vilivyokopa virejeshe mikopo kwa wakati.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chalinze Zainabu Makwinya alisema, kwa kipindi kinachoishia Juni 2019 mapendekezo ya hoja za Ukaguzi yaliyotolewa yalikuwa 44 , yaliyotekelezwa na hoja kufungwa ni 18 sawa na asilimia 41 na yanayoendelea kufanyiwa kazi kulingana na hoja ya mkaguzi ni 26 sawa na asilimia 59.

Zainabu ambaye ni Afisa Elimu msingi wa Halmashauri hiyo alisema kwa hesabu za mwaka 2018/2019 Halmashauri hiyo imepata hati ya ukaguzi inayoridhisha.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.