• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Pinda aipongeza Pwani Ujenzi wa Viwanda

Posted on: August 3rd, 2023

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda ameupongeza Mkoa wa Pwani kwa kuwa kinara katika ujenzi wa uchumi wa viwanda nchini.

Akifungua Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki mjini Morogoro, Mhe. Pinda ameeleza kuwa hakuna zao ambalo halikubali katika Kanda hiyo kwa kuwa Kanda hiyo ina hali ya hewa tofauti tofauti.

Ameeleza kuwa kauli mbiu ya Maonesho hayo isemayo "Vijana na Wanawake ni Msingi wa mifumo endelevu ya Chakula" inaakisi ukweli kuwa wanawake ni jicho muhimu katika Chakula ikiwemo lishe kwa watoto huku akifafanua kuwa kwa vijana ni lazima waanze jitihada leo ikiwemo kukabiliana na changamoto za kilimo na mfumo wake uwe wa mashamba makubwa na yenye tija na akabainisha kuwa kwa mujibu wa takwimu za sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022, Kanda ya Mashariki ina vijana asilimia 36 ambayo iko juu ya asilimia ya Taifa ya asilimia 34, hivyo ni muhimu wakiandaliwa vyema kushiriki katika mifumo ya uzalishaji na kuliletea taifa maendeleo.

Mhe. Pinda ametoa rai kwa viongozi wa Mikoa ya Kanda ya Mashariki Kujipanga na programu ya Mradi wa "Build Better Tomorrow" Kwa kuainisha mashamba watakayopewa vijana pale ambapo watajitokeza kutaka kujiendeleza katika sekta hizo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge akitoa salaam za Mkoa na Kanda ya Mashariki ameeleza kuwa matarajio ya Mikoa hiyo ni kuhakikisha kuwa matarajio na matamanio ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan yanafikiwa na akaongeza kuwa yeyote mwenye shaka na jitihada na kazi za Mhe Rais afike katika mikoa hiyo kujionea na kushuhudia hayo.

Akiuelezea Mkoa wa Pwani, Mhe. Kunenge amesema kuwa unaendelea kuhakisha vipaumbele vyake ni sahihi na vipaumbele hivyo ni Vipaumbele vya Mhe Rais.

Amesema juhudi za Mkoa wa Pwani ni kuanzisha mazao mapya ikiwemo Michikichi na Mpunga na kuwa mazao ya Ufuta na Korosho yameendelea kufanya vizuri katika Mkoa huo ikiwemo kiwango cha ubora wa daraja la kwanza kufikia asilimia 92 kwa msimu uliopita.

Ameeleza kuwa washiriki wa maonesho ya nane nane ya mwaka huu wa 2023 wameongezeka kutoka watu 477 hadi 589 ikiwa ni ongezeko la asilimia 22 na kuwa dhamira ya Mikoa ya Kanda ya Mashariki ni kuchangia katika kulisha Tanzania na Dunia nzima.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.