• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Program ya BBR kuongeza Chakula ,ajira _Rais Dkt Samia

Posted on: August 29th, 2023

Serikali imesema itaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kilimo kupitia mpango wa kutengeneza kesho iliyobora yaani ‘BBT’ kwa vijana ili kuwa na idadi kubwa ya kundi hilo ambalo litasaidia upatikanaji wa uhakika wa chakula na kuongeza wigo wa kujiajiri.

Hayo yamesemwa a Agosti 27, 2023 na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akifunga mafunzo ya Uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa Tanzania bara yaliyofanya kwenye ukumbi wa chuo hicho kilichopo Halmshauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani ambayo yamefanyika kwa siku sita kuanzia Agosti 22 hadi 27.

Amesema tayari serikali inatekeleza program mbalimbali za kilimo zinazowahusu vijana na kwamba muitikio ni mkubwa wa kujihusisha na kilimo ambacho amedai kinatoa fursa nyingi za vijana kujiajiri na kujipatia kipato.

Ameongeza kuwa katika kufanikisha hayo wakuu wa mikoa na makatibu tawala wamejengewa uwezo na kulisaidia kundi ili kuzitumia vyema fursa zinazopatikana katika maeneo yao kupitia kilimo.

“Kupitia program yetu ya Jenga kesho iliyobora yaani Building Better Tomorrow (BBT) ambayo inaratibiwa na Wizara ya Kilimo pamoja na ya Mifugo tumewajengea uwezo vijana wengi namna ya kulima kilimo chenye tija na ufugaji wa kisasa, tayari baadhi yao wamefuzu masomo na tayari wameanza kazi katika maeneo yao ni muhimu sasa wakuu wa mikoa muwasaidie amesema Dkt. Rais Samia Suluhu Hassan.

Aidha amewataka wakuu wa mikoa na makatibu tawala kutatua kero zote za wananchi hususani suala migogoro ya ardhi ambalo limekuwa ni tatizo kubwa katika baadhi ya mikoa.

Awali Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa alisema ili kufikia malengo ya Serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi ni wakuu wa mikoa kusimamia kikamilifu miradi na ikamilike kwa wakati.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  Godfrey Chongolo, akitoa salaam za Chama hicho wakati shughuli hiyo, amesema kuwa mafunzo hayo yatakuwa chachu ya kuongeza morali ya utendaji kazi kwa viongozi hao, ili kuleta ufanisi na tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

“Mhe. Rais, Chama Cha Mapinduzi ndiyo tuliopewa dhamana na wananchi mwaka 2020, kushika dola, kuunda Serikali na kusimamia na kuongoza nchi. Mafunzo haya ambayo yametolewa kwa Viongozi na watumishi wa Serikali yatawaweka kwenye utayari wa kutoa huduma bora na zenye ufanisi mkubwa.

“Tunakupongeza sana wewe kwa kutoa fursa ya mafunzo haya. Tunampongeza Waziri wa TAMISEMI na watendaji wote wa wizara kwa mafunzo haya. Tuliahidi kwa wananchi mwaka 2020 kuwa Serikali tutakayoiunda na kuisimamia itatoa huduma bora. Kundi hili ni kundi muhimu sana katika utekelezaji wa Ilani, maana ndilo linalopokea mafungu yote ya miradi na shughuli za maendeleo kwa ajili ya wananchi,” amesema Ndugu Chongolo.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.