• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Pwani kutenga maeneo Kilimo cha kisasa

Posted on: January 26th, 2024

Serikali Mkoani Pwani imeweka mikakati kabambe ya kutenga maeneo kwa ajili ya kilimo cha kisasa na chenye tija ambacho kitajumuisha mazao ya kibiashara kwa lengo la kukuza uchumi.

Hayo yamebainishwa leo January 26, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Alhaji Abubakari Kunenge wakati wa halfa fupi ya kukabidhi matreka matatu kwa uongozi wa halmashauri ya Wilaya ya Kibaha.

Katika hafla hiyo, Kunenge amesema kwamba matreka hayo matatu ambayo wamepatiwa na Rais Dkt. Samia yatakuwa msaada mkubwa katika kuleta mapinduzi kwenye kilimo cha kisasa.

"Sisi kama Mkoa wa Pwani tumejipanga kuhakikisha kwamba tunajikita zaidi katika kuboresha sekta ya kilimo na kwa sasa tumepokea matreka haya kwa ajili ya halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, hivyo hatuna budi kumshukuru Rais wetu kwa hatua hii ya kutupatia matreka haya," amesema.

Amefafanua kwamba katika kumuunga mkono Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa sasa wameanza kujikita katika kilimo cha mazao ya biashara yakiwemo mazao ya Pamba, ufuta, michikichi, korosho mihogo pamoja na mazao mengine ambayo yataweza kuleta mabadiliko katika kukuza uchumi.

Kunenge ameeleza kwamba Mkoa wa Pwani unataka kufanya mabadiliko makubwa katika sekta ya kilimo hivyo ana imani kubwa juu ya mabadiliko hayo katika halmashauri zote tisa zilizopo katika Mkoa wa Pwani.

Amewaomba viongozi wa halmashauri hiyo kuhakikisha kwamba wanayatunza vizuri matrekta hayo ili yaweze kudumu kwa kipindi kirefu ili kuweza kuwasaidia wakulima katika kilimo cha biashara.

Ameongeza kuwa katika kuendana na kasi ya mabadiliko Wilayani ya Rufiji, tayari kumeshafanyika uzinduzi wa zao la pamba na kwamba kutajengwa kiwanda kikubwa kwa ajili ya kuchakata zao hilo.

Sambamba na hayo, amempongeza kwa dhati Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake za hali na mali katika kukuza sekta ya kilimo na kuwezesha upatikanaji wa matreka hayo.

Pia amesema kuwa wapo katika mikakati ya kujenga skimu kubwa za umwagiliaji ambazo zitaweza kuwasaidia wakulima katika kuendesha shughuli zao za kilimo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Saimon amesema kwamba wameshakubaliana kuwa matrekta hayo yanakabidhiwa katika halmashauri ya Wilaya ya kibaha ili kuboresha kilimo cha kisasa.

Mkuu huyo wa Wilaya amebainisha kwamba katika mpango wao wamekubaliana mambo matatu ikiwemo kuunganisha kilimo pamoja na viwanda, rasilimali watu pamoja na teknolojia lengo likiwa ni kuwasaidia wakulima kulima kilimo cha kisasa.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Erasto Makala ameishukuru Serikali kwa kuweza kuwapatia matrekta hayo ambapo amesema kuwa lengo lao kubwa ni kutoka katika kilimo cha chakula na kujikita katika kile cha biashara.

Mkoa wa Pwani kwa sasa umejipanga kuunganisha kilimo pamoja na viwanda lengo ikiwa ni kutimiza azma ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hasssan kulisha dunia nzima kupitia sekta ya kilimo.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.