• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Pwani yanufaika na awamu ya Pili unaofadhiliwa na korea Foundation For Health cara (KOFIH)

Posted on: June 22nd, 2023

Halmashauri Tisa , Mkoani Pwani zinatarajia kunufaika na awamu ya pili ya Mradi unaofadhiliwa na Korea Foundation For Health Care (KOFIH ),mradi ambao unaolenga kupunguza vifo vya uzazi kwa mama na mtoto mchanga.

Mradi huu unatarajia kutekelezwa katika kipindi cha miaka mitano na kugharimu takriban Bilioni 12 baada ya kukamilisha utekelezaji wa miaka Saba (2016-2022).

Akizungumza wakati wa tathmini ya Mradi huo awamu ya kwanza (2016-2022), Mkurugenzi wa huduma za afya ya uzazi na mtoto Wizara ya Afya Dkt.Ahmad Makuwani alieleza, mradi huo umetekelezwa katika Halmashauri sita ,vituo 19 chini ya Wizara ya afya na mkoa wa Pwani na uligharimu dollar za Kimarekani 5 milioni (USD).

Makuwani alisema, mradi umeleta matokeo chanya kwa kupunguza changamoto ya vifo vya uzazi na motto, kwani kabla ya Mradi kulikuwa na vifo vya watoto 800 hadi Mradi unakamilika vifo vimefikia 390.

Kwa Upande wa vifo vya Mama ilikuwa vifo 82 na hadi mradi unamalizika vifo vimefikia 35.

Awali Mratibu wa afya ya uzazi na mtoto Kanda ya Mashariki na Mkoa wa Pwani ,Joyce Gordon alifafanua ,KOFIH imeongeza majengo ya uzazi ,mama na mtoto, kununua vifaa mbalimbali vya uzazi,vitanda,majokofu ya kuhifadhia damu,kujenga vyumba vya kufulia na kusomesha wataalam wa kutoa dawa za usingizi.

Alieleza, suala la kukosa usafiri ni moja ya chanzo kinachosababisha mama kufariki njiani wakikimbizwa kujifungua ,hivyo KOFIH wametoa magari ya wagonjwa matano Kibaha Mjini, Kibiti, Kisarawe,Mafia, Rufiji huko Mbwera wamepatiwa boti .

Nae Mjumbe Mwakilishi kutoka KOFIH Tobias Kyuong Kyun Oh alielezea,wanaanza mradi mwingine utakaotekelezwa kwa miaka mitano ijayo na mradi huo utagharimu takriban Bilioni 12 za kitanzania.

Kyun Oh alieleza ,mradi huu utanufaisha akinamama wote watakaokwenda kujifungua katika Halmashauri zote Tisa Mkoani Pwani.

“Tunaunga mkono juhudi za Serikali chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ambae anaonyesha Nia kubwa ya kupunguza changamoto ya vifo vya uzazi kwa mama na mtoto, na sisi tunaendelea kushirikiana na Serikali kuboresha huduma katika sekta ya afya”

Kwa Upande wake,mganga mkuu wa mkoa wa Pwani Dkt.Gunini Kamba alieleza,mkoa unaendelea kupunguza changamoto za uzazi na kuboresha huduma za kiafya.

Gunini aliwashukuru KOFIH kwa kushirikiana na mkoa kuboresha huduma na kupambana na kero zinazochangia kusababisha vifo hivyo.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.