• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Pwani yatekeleza Maagizo ya Rais Samia

Posted on: November 11th, 2022

Mkoa wa Pwani umetekeleza maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ya kusafisha Bonde la Mto Ruvu ili kuwezesha upatikanaji wa maji kwa matumizi ya binadamu.

Hayo yameelezwa leo Novemba 9, 2022 na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge wakati akitoa taarifa kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philip Isdory Mpango juu ya hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Mkoa huo zikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan yanayolenga kuondoa changamoto ya upungufu wa maji kwenye bonde hilo unaosababishwa na shughuli za kibinadamu.

Mhe. Kunenge alisema kuwa ukaguzi wa Bonde hilo ulifanyika Novemba 2 na 3, 2022 kwa kutumia "Helkopter" na kubaini uwepo wa mifugo mingi huku kukiwa na uchepushaji Maji kwenye baadhi ya maeneo na kuwa tayari hatua zimechukuliwa kudhibiti hali hiyo.

"Baada ya kubaini hayo, tuliamua kuwaelekeza wale wote wanaotumia maji kuendesha kilimo cha umwagiliaji kwa njia halali (wenye vibali) wasitishe kwa muda, wasio na vibali pamoja na wenye mifugo kuacha mara moja na wameacha, lakini Operesheni zinaendelea, na kukamata watumiaji wasio na vibali na watakaokaidi maagizo na maelekezo haya," alifafanua Kunenge.

Akielezea taratibu walizotumia kufanikisha zoezi hilo, Mhe. Kunenge alibainisha kuwa ofisi yake ilitumia utaratibu mzuri wa kufanya mikutano na wadau mbalimbali iliyosaidia kubaini na kuthibiti uchepushaji wa Maji na kuzuia Ukataji Miti ili kutunza vyanzo vya maji.

"Katika kutekeleza Maagizo ya Mhe. Rais, niliitisha Mkutano wa Viongozi wa Mkoa ulioshirikisha Chama cha Wafugaji, Chama cha Wavunaji Mkaa, Viongozi wa Bonde la Wami RUVU na Wakala wa Huduma za Misitu na nnashukuru Waziri wa Maji alihudhuria na kikao hicho kikaweka mikakati ya kuhifadhi mazingira kwa kutoharibu vyanzo vya maji na kuzuia ukataji haramu miti."

Kuhusu udhibiti ukataji miti na kuchoma mkaa ovyo, Mhe. Kunenge alieleza kuwa mkoa wa Pwani umeazimia kudhibiti vyombo vya usafiri (pikipiki) vinavyobeba Mkaa kwa kuvisajili na kuvifuatilia kujua wanakotoa huo mkaa na kuwa wanapanga kuja na mpango wa kudhibiti uvunaji wa Mkaa kwa kupunguza utoaji vibali vya mkaa na hili litahamasisha matumizi ya nishati Safi ya gesi.

Kwa upande wa Ufugaji, alieleza kuwa kuna changamoto kubwa ya Mifugo vamizi na hasa katika kipindi hiki cha Ukame ambacho hata Mifugo iliyopo kwenye maeneo hayo wanatafuta maji.

"Katika hili, viongozi kutoka kwenye Mikoa yenye mifugo mingi tumekubaliana kuwa wafugaji wabakize mifugo yao kwenye maeneo yao na itambuliwe ili kuweka mikakati ya upatikanaji Malisho na Maji huku mikakati ya kuhuwisha matumizi bora ya ardhi, kuanzisha na kutumia Ranchi ndogo ndogo ikiendelea.

Makamu wa Rais alitembelea chanzo na mitambo ya maji ya Ruvu chini iliyopo katika Kijiji cha Kongo Kata ya Yombo Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani kujionea hali ya upatikanaji wa maji ulivyo kwenye Bonde la Mto Ruvu unaotegemewa na Mikoa ya Pwani na Dar es Salaam.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.