• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Pwani yaweka mkakati ushiriki utekelezaji Mradi wa Umeme mto Rufiji

Posted on: April 11th, 2019

Kamati ya Amani ya Mkoa wa Pwani imetembelea eneo la Mradi wa Umeme wa mto Rufiji na kufanya maombi maalum ili utekelezaji wake ukamilike kwa ufanisi na kwa wakati uliopangwa.

Kamati hiyo yenye wajumbe kutoka madhehebu mbalimbali imeshiriki kwenye ziara ya siku tatu iliyoanza April tisa ikijumuisha Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Pwani na ya Wilaya ya Rufiji, Wakuu wa Wilaya sita, Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji pamoja na Viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Mloka.

Wakiwa katika eneo la mradi, msafara huo ulioongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo ulipokea maelezo ya utekelezaji wa mradi huo mkubwa wa kimkakati kutoka kwa Wataalamu wa Shirika la Umeme nchini-TANESCO wanaosimamia mradi huo.

Akifafanua lengo la ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo alieleza kuwa sehemu ya eneo la ujenzi wa mradi liko katika Mkoa wa Pwani hivyo ni wajibu wa jamii kuwa na uelewa mpana na wajibu wa kushiriki katika utekelezaji na kulinda miundombinu yake ikiwa ni pamoja na kubaini changamoto zilizopo au zinazoweza kujitokeza na kuzipatia ufumbuzi.

“Asilimia kubwa ya shughuli za utekelezaji wa mradi huu zitakuwa katika eneo la Mkoa wa Pwani hivyo tunataka tuone namna ambavyo Kamati ya Ulinzi na Usalama na Kamati ya Amami itashughulikia maswala yote yaliyoko ili mradi huu usikwame” amesema Mhandisi Ndikilo.

Mkuu wa Mkoa ameongeza kuwa pamoja na kuwa wataalamu wa kitanzania na Mkandarasi wako kwenye eneo la utekelezaji wakiendelea na majukumu yao, bado kuna mambo mengine nje ya eneo hilo ambayo Mkoa kwa kushirikiana na Taasisi nyingine zinawajibu wa kuyasimamia ili kuhakikisha kuwa utekelezaji unafanikiwa na kwa wakati.

Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Bibi. Theresia Mmbando (aliyeshika mic) akitambulisha msafara wa Kamati ya Ulinzi na Usalama na ile ya Amani zote za Mkoa wa Pwani mara baada ya kufika kwenye eneo la Mradi wa Umeme wa mto Rufiji


Mhandisi Joseph Kiyumbi wa TANESCO (wa kwanza mbele aliyevaa shati jeupe) akitoa maelezo ya utekelezaji wa Mradi kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na kamati ya Amani Mkoa wa Pwani

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akifafanua Mkakati wa Mkoa katika kufanikisha utekelezaji wa Mradi wa Umeme wa mto Rufiji wakati wa ziara ya Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na kamati ya Amani Mkoa zilizotembelea eneo la mradi huo.


Mhandisi Joseph Kiyumbi wa TANESCO (aliyevaa kofia nyeupe) akitoa maelezo ya utekelezaji wa Mradi kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na kamati ya Amani Mkoa wa Pwani


Mhandisi Joseph Kiyumbi wa TANESCO (wa pili toka kushoto) akimuogoza Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo (wa kwanza toka kulia) na msafara wake kutembelea eneo la  utekelezaji wa Mradi

Mhandisi Mwanji Yohana wa TANESCO (mwenye kofia Nyeupe) akimuogoza Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo (mwenye karatasi mkononi) na msafara wake kutembelea eneo la  utekelezaji wa Mradi


Msafara ukiwa katika moja ya maeneo ya utekelezaji Mradi

 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo (wa Pili toka kushoto mbele) akifuatilia maelezo ya Mradi toka kwa Mhandisi Joseph Kiyumbi wa TANESCO (aliyevaa kofia nyeupe) 


Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo (wa Pili toka kushoto mbele) akielekeza jambo kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na kamati ya Amani Mkoa wa Pwani


Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.