• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Rais Samia kuzindua Bandari Kavu ya Kwala na miradi mikubwa ya miundombinu Mkoani Pwani.

Posted on: July 22nd, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Bandari Kavu ya Kwala, Mkoani Pwani, Julai 31, 2025.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 22, 2025 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Abubakar Kunenge, amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kushuhudia tukio hilo kubwa la kihistoria.

Katika ziara hiyo, Mhe. Rais Samia atazindua rasmi safari za Treni ya Mizigo kwa njia ya Reli ya Kisasa (SGR), kupokea mabehewa ya mizigo kwa njia ya Reli ya Zamani (MGR), pamoja na kuzindua Kongani ya Viwanda ya Kwala (Kwala Industrial Park), moja ya maeneo ya viwanda makubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki.

“Mhe. Rais atafanya uzinduzi rasmi wa safari za treni ya mizigo ya mwendo kasi kupitia Kituo Kikuu cha Kuunganishia Mabehewa ya Mizigo na Karakana ya Treni za Mizigo (Marshalling Yard) kilichopo Kwala,” alisema Mhe. Kunenge.

Aliongeza kuwa uzinduzi huo ni matokeo ya juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuwekeza kwenye miundombinu ya kisasa ya viwanda, reli na bandari ili kuongeza tija na ufanisi katika sekta ya uchumi.

Kuhusu Bandari Kavu ya Kwala, Mhe. Kunenge alisema kuwa mradi huo utakuwa na uwezo wa kuhudumia wastani wa makasha ya mizigo 823 kwa siku, sawa na makasha 300,000 kwa mwaka. Hii itasaidia kupunguza msongamano katika Bandari ya Dar es Salaam kwa wastani wa asilimia 30.

Akifafanua zaidi, alisema kuwa Mhe. Rais Samia atapokea jumla ya mabehewa 160 ya mizigo, ambapo mabehewa 100 ni mapya yaliyonunuliwa na Serikali kwa ajili ya MGR, mabehewa 20 yamefanyiwa ukarabati, na mengine 40 yametolewa na Shirika la Chakula Duniani (WFP).

Kwa upande wa Kongani ya Viwanda ya Kwala, ambayo ni miongoni mwa maeneo ya viwanda makubwa zaidi Afrika Mashariki, Mhe. Kunenge alisema kuwa Mhe. Rais atazindua viwanda saba vilivyokamilika na vinavyoendelea na uzalishaji, pamoja na viwanda vitano ambavyo vipo katika hatua mbalimbali za ujenzi. Kongani hiyo inatarajiwa kuwa na zaidi ya viwanda 250.

Hafla hiyo inatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa na kimataifa, huku Mhe. Rais akitarajiwa pia kufanya mkutano mkubwa na wananchi mara baada ya shughuli za uzinduzi kukamilika.

Miradi inayotarajiwa kuzinduliwa inaonyesha dhamira ya dhati ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuimarisha sekta ya uchukuzi na usafirishaji, na kuifanya Kwala kuwa kitovu cha biashara na uchukuzi wa kimataifa (International Logistic Hub).

Aidha uzinduzi huo utaleta manufa makubwa yakiwemo kuongeza mapato, kukuza usafiri wa Reli, kupunguza uharibifu wa barabara, kutunza manzingira na kuongeza ushindani wa kikanda na Ushirikiano wa kikanda  na nchi za jirani kama vile DRC, Zambia, Rwanda,Burundi, Malawi, Zimbabwe, Uganda, na Sudani ya Kusini.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Rais Samia kuzindua Bandari Kavu ya Kwala na miradi mikubwa ya miundombinu Mkoani Pwani.

    July 22, 2025
  • Pwani Yazindua Kampeni ya Ugawaji wa Vyandarua Bure Zaidi ya 971,000 kwa Vita Dhidi ya Malaria.

    July 18, 2025
  • Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Aongoza Ufunguzi wa Kikao cha Mpango wa MTAKUWWA II.

    July 18, 2025
  • Utekelezaji TIRP2 wa TRC unamanufaa kwa jamii - Nsajigwa.

    July 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.