• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RAS Pwani ahimiza uadilifu na usimamizi wa shughuli za TASAF

Posted on: June 30th, 2022

Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Mhandisi Mwanasha Tumbo amewaagiza waratibu na wasimamizi wa fedha za Mpango wa Kunusuru Kaya za Walengwa unaosimamiwa na Mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF) kuimarisha usimamizi, kuwa waadilifu na waaminifu kwa fedha zinazotolewa kwa ajili ya wanufaika.

Mhandisi Mwanasha ameyasema hayo wakati akifungua kikao kazi cha kujadili shughuli za mpango kazi wa Mpango huo kwa mwaka 2021/2022 kilichowahusisha wakuu wa idara na vitengo kutoka Sekretariet ya Mkoa na waratibu wa TASAF wa Halmashauri zote za mkoa wa Pwani.

Alisema kuwa jumla ya kaya za Walengwa 29,683 zinanufaika kupitia mpango huo Mkoani Pwani ambapo sh. Bilioni 5.609 zimeshapokelewa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 hivyo ni lazima zisimamiwe ili kutimiza azma ya Serikali na kujiepusha na migongano.

Mhandisi Mwanasha ameeleza kuwa yapo malalamiko kutoka kwa wanufaika Kuwa wakati mwingine fedha hizo haziwafikii, jambo ambalo linachafua mpango mzima wa utekelezaji na akafafanua kuwa malalamiko hayo yanajitokeza kutokana na kuwaachia watendaji na wenyeviti wa vijiji fedha ambapo zinachelewa kuwafikia walengwa.

"Hata huu utaratibu wa Sasa wa kuwalipa walengwa fedha kwenye simu nao una changamoto kwa kuwa walengwa wengine hawajui matumizi ya mitandao ya simu, utakuta mtu anamuagiza mjukuu wake, jirani ama jamaa hadi fedha ikitoka unakuta mlengwa anapata pungufu ama wananufaika ambao hawastahili,” alisema Mhandisi Mwanasha.

Mhandisi Mwanasha aliendelea kusema, "Tuhakikishe kuwa fedha hizi zinawafikia walengwa ili kutimiza azma ya Serikali kusaidia Kaya za Walengwa, Mimi ni shuhuda, nilifika pale Kimaramisale ambako ni kati ya Vijiji vipya vilivyoongezwa kwenye Mpango, tumefika pale watu wakapokea fedha zao na kuishukuru Serikali kwani haijawahi kutokea kwao.”

Kutokana na changamoto hiyo Mwanasha ameelekeza waangalie namna ya kutoa elimu ya Utaratibu huo ili Hali wahusika wapate Uelewa.

Katibu Tawala huyo alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kuwapigania wananchi wa Hali ya chini ili wapate msaada .

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji mkoa , mratibu wa TASAF Mkoani Pwani Roselyn Kimaro alieleza kuwa mbali na kaya kunufaika na fedha, pia ipo miradi 168 yenye thamani ya sh. Bilioni 1.084 iliyoibuliwa na wananchi ambayo inatekelezwa na walengwa na inaendelea vizuri.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.