Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Pili Mnyema amesisitiza umuhimu wa watumishi kuwajibika kwa kufanya kazi kwa uadilifu, kuzingatia kanuni, taratibu, sheria na miongozo ya utumishi wa Umma.
Mnyema ametoa msisitizo huo leo Novemba 18, 2025 wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Chalinze ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kuzitembelea Halmashauri zote za Mkoa huo inayohusisha pia ukaguzi wa miradi ya maendeleo.
"Uadilifu ni pamoja na kuwa mnyenyekevu, kuepuka rushwa, ubadhirifu na kutosababisha maumivu kwa watumishi mwenzako," alisema.
Pia amesisitiza watumishi kuzingatia ushirikiano, upendo, kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wananchi.
"Kama watumishi wa Umma tunawajibu mkubwa wa kuweka malengo halisi ambayo yatakidhi matarajio ya Wananchi na si kuwa miungu watu" aliongezea.
Alisistiza pia kuhusu uzingatiaji matumizi ya mifumo ya Serikali ukiwa ule mfumo wa upimaji wa utendaji kwa watumishi PEPMIS.
"Tunafahamu kuwa Dunia inakwenda kasi sna kulingana na Teknolojia na Serikali imeanza kutumia mifumo hiyo hivyo tunapaswa kwenda sambamba na mifumo hiyo" alisema
Katika ziara hiyo, Mnyema alipata fursa ya kutembelea na kukagua miradi ambayo ni mradi wa Ujenzi na uendelezaji wa miundombinu ya Hospitali ya Msoga pamoja na Mradi wa vyumba vya Biashara (fremu) katika kituo cha mabasi cha chalinze.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
Sanduku la Posta: 30080 Kibaha
Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500
Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500
Barua pepe: barua@pwani.go.tz
Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.