• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Rc Amshukuru Rais Samia kwa Mradi wa Biliion 14.98 Umeme Vijijini

Posted on: September 25th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuleta mradi wa umeme vijijini wenye thamani ya zaidi ya bilioni 14.98 mkoani Pwani. Mradi huo unatarajiwa kuboresha maisha ya wananchi na kurahisisha upatikanaji wa umeme vijijini.

Mhe. Kunenge alitoa shukrani hizo leo wakati wa tukio la makabidhiano ya mradi kati ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na mkandarasi wa mradi, China Railway Construction Electrification Bureau Group (CRCEBG), lililofanyika katika ukumbi mdogo wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani.

Mradi huo unalenga kunufaisha vitongoji 2,045, ambapo tayari vitongoji 1,135 vimenufaika. Kwa sasa, mradi unaendelea na utawanufaisha wakazi wa vitongoji 135 vilivyobaki, ambavyo vinatarajiwa kukamilika ndani ya miaka miwili, kufuatia maelekezo ya Ilani ya CCM inayolenga kufikia upatikanaji wa umeme kwa asilimia 100 kwa wananchi.

Mhe. Kunenge pia ameagiza mradi huo kutambulishwa katika wilaya zote za Mkoa wa Pwani ambazo vitongoji vyake vitanufaika, ili kuwezesha ufuatiliaji na kuhakikisha utekelezaji unafanyika kwa ufanisi.

Aidha, amemshauri mkandarasi wa mradi kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kutoa taarifa za changamoto zinazoweza kujitokeza ili zitafutiwe suluhisho haraka.

"Naomba mradi ukamilike kwa wakati, msisukumwe, lakini mkihitaji kusukumwa nitawasukuma, kwani nitawatembelea mara kwa mara," alisema Mhe. Kunenge.

Pia, Mhe. Kunenge amesisitiza umuhimu wa kuharakisha usambazaji wa umeme kwenye maeneo ya visiwani ili kuchochea maendeleo ya uchumi wa bluu, kuongeza mapato ya serikali, na kukuza sekta ya utalii.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa REA Vijijini, Mhandisi Jones Olotu, alisema kuwa mradi huo unalenga kunufaisha vijiji vyote vya Mkoa wa Pwani ifikapo mwaka 2025.

Afisa Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Bi. Felister Edwin, kutoka China Railway Construction Electrification Bureau Group (CRCEBG), akizungumza kwa niaba ya mkandarasi, aliahidi kufanyia kazi maelekezo ya Mkuu wa Mkoa na kuhakikisha mradi unakamilika kwa ufanisi na kwa wakati uliopangwa.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.