• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenenge aelekeza TEMESA kuwasilisha Mpango matengenezo kivuko Mafia

Posted on: March 3rd, 2023

Mkuu wa mkoa wa Pwani alhaj Abubakari Kunenge ameelekeza Wakala wa ufundi na umeme (TEMESA) kuwasilisha kwa wananchi, serikali ya wilaya na ya mkoa taarifa yenye mpango wao wenye gharama halisi za matengenezo na uwezo wa kivuko kipya kitakachotoa huduma kwa wananchi wa mafia.

Alitoa maelekezo hayo katika kikao cha Bodi ya barabara Mkoa kilichofanyika leo Mach 3, 2023 kwenye ukumbi wa mikutano wa jengo la ofisi yake baada ya kupata maelezo ya Meneja wakala wa ufundi na umeme (TEMESA) Mkoa wa Pwani Mhandisi Rehana Juma alieleza kuwa vivuko vya MV Kilindoni inafanyiwa marekebisho ya kimatengenezo kwa gharama ya zaidi ya sh. milioni 294 na imefikia asilimia 85 ya matengenezo tayari kwa majaribio ili iingie majini kuanza safari zake na kuwa kutokana na matengenezo ya mara kwa mara ya vivuko vilivyopo, Wizara husika na TAMESA imeamua kuanza mchakato wa kununua kivuko kipya chenye uwezo wa kubeba Tani 120 za mizigo na watu 500, kwa thamani ya Sh. Bilioni 9 ili kupunguza adha ya ongezeko la wasafiri wa pande zote mbili za Nyamisati na Mafia.

"Niwaombe TEMESA msifanye usiri katika hili, wananchi wanapaswa kushirikishwa ili nao watoe maoni yao kujua endapo kivuko hicho kitawafaa, haiwezekani leo mnakuja na mpango wenu, na kusema mnaleta kivuko cha zaidi ya shilingi Bilioni 9 wakati hamjashirikisha mkoa, wilaya wala wananchi, muda mwingi wananchi wanakosa usafiri kwa kuwa vivuko vinakuwa kwenye matengenezo na kusababisha abiria kukwama na wanaoathirika zaidi ni wananchi wa wilaya ya Mafia ambao wanauhitaji wa kivuko cha uhakika kitakachoweza kujibu kero ya usafiri na usafirishaji inayowakabali." alisisitiza Kunenge.

Aliendelea kusema kuwa wakati serikali ikiendelea kuufungua mkoa kwa miundombinu mbalimbali ya barabara na reli, pia kuna haja ya kupata ufumbuzi wa muda mrefu kutatua changamoto ya usafiri hasa wa njia ya maji.

Kunenge pia aliitaka Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) nayo kuwasilisha kwa serikali ya mkoa mpango wake wa maboresho yanayohitajika na namna yatakavyotekelezwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mafia Juma Salum alieleza kilio cha usafiri wa uhakika ni mtihani mkubwa kwa wana Mafia akifafanua kuwa sasa ni siku ya tatu wasafiri wa Mafia wamekwama Nyamisati kutokana na kukwama kwa usafiri na kuwa sasa imepita takriban miezi mitano ikiwa kivuko cha MV Kilindoni kikidaiwa kuwa katika matengenezo suala ambalo linakatisha tamaa katika maendeleo ya Mafia.

"Kivuko hiki hakijibu tatizo la usafiri Mafia, tunatakiwa kupata uhakika wa usafiri wa kuingia Nyamisati na Kutoka Mafia, kuwe na mpango wa muda mrefu, kwa shida hizo kunasababisha wananchi kuhitaji huduma ya kivuko cha binafsi kilichokuwepo zamani ili kiwasaidie," alisema Salum.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.