• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge: Aagiza Mradi wa IPOSA ulete Matokeo yanayoonekana.

Posted on: October 2nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, ameielekeza Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kuhakikisha programu ya IPOSA (Integrated Programme for Out-of-School Adolescents) inakuwa na matokeo chanya kwa kuwajengea vijana uwezo wa kujiajiri na kuajirika.

Akifunga mafunzo ya walimu wa programu hiyo yaliyofanyika katika  Ukumbi wa mikutano Manispaa ya Kibaha, mkoani humo,  alisisitiza elimu inayotolewa kupitia IPOSA haipaswi kubaki kwenye vyeti pekee, bali iwe chachu ya mabadiliko katika maisha ya wahitimu.

“Mradi huu lazima uwe na matokeo ya kweli, vijana wanapaswa kufundishwa stadi zitakazowawezesha kujitegemea kiuchumi, pamoja na kupunguza idadi ya watu wazima wasijua kusoma na kuandika, Hii ndiyo maana halisi ya elimu yenye tija,” alisisitiza Kunenge.

Vilevile Kunenge alimuagiza Afisa Elimu wa Mkoa kusimamia kikamilifu utekelezaji huo na kuhakikisha unaacha alama katika maisha ya vijana wanaonufaika nao.

“Nakuagiza Afisa Elimu Mkoa kuhakikisha kuwa programu ya IPOSA inaleta matokeo yanayoonekana kwa vijana na jamii kwa ujumla, tunahitaji kuona ushahidi wa mafanikio,” alifafanua Kunenge.

Programu ya IPOSA inalenga kuwafikia vijana waliopo nje ya mfumo rasmi wa elimu kwa kuwapatia ujuzi na maarifa mbalimbali, yakiwemo mafunzo ya stadi za maisha, ujasiriamali, kusoma, kuandika, kuhesabu na mafunzo ya amali, ili kuwawezesha kujitegemea kiuchumi.

Mafunzo hayo yamekuwa yakitekelezwa katika mikoa mbalimbali nchini kwa lengo la kuhakikisha kundi la vijana lisilofikiwa na mfumo wa kawaida wa elimu linapewa nafasi ya kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge: Aagiza Mradi wa IPOSA ulete Matokeo yanayoonekana.

    October 02, 2025
  • Mkoa wa Pwani Waendelea Kung’ara katika Utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF).

    September 30, 2025
  • Rais Samia Aipongeza Pwani Kwa Kuibeba Vyema Ajenda ya Kitaifa ya Uwekezaji Katika Viwanda.

    September 28, 2025
  • Serikali Yatoa Bilioni 19.8 Kujenga Soko la Kisasa na Barabara Mbili Kibaha.

    September 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.