• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge aelekeza Madiwani Mafia kupewa Mafunzo

Posted on: June 13th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa PWANI Abubakar Kunenge ameielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Mafia kuwapatia Wahe. Madiwani wa Halmshauri hiyo Mafunzo ya Uchumi ili waweze kuwa Wabunifu wa vyanzo vipya vya mapato na kutumia Ipasavyo Fursa za Uchumi na Uwekezaji katika Halmshauri yao.

RC kunenge ametoa maelekezo hayo leo Juni 13, 2022 wakati wa Kikao Maalumu cha Baraza la Madiwani cha Kujadili Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kilichofanyika Ukumbi wa Magereza Wilayani Mafia.

Katika maelekezo hayo, Mhe. Kunenge amewaeleza madiwani hao kuwa wanatakiwa kwenda na Spidi ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ambae spidi yake ya kutafuta Wawekezaji imekuwa kubwa na yenye mafanikio.

“Pangeni mikakati Mipya ya Kuongeza Mapato na kukuza Uchumi, kama Mikakati ni ile ile Bajeti ni ile ile hatuwezi kuwa na matokeo mapya kwa kuwa Bajeti ni mipango unayoipa gharama. Amesema RC Kunenge.

Ameeleza kuwa Zamani Halmashauri zilikuwa zinapata Ruzuku Kubwa lakini kwa sasa Serikali imewapa Miradi Mikubwa ya Kimkakati na halmashauri kutakiwa kuibua vyanzo vipya Ili iweze kujiendesha.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Pwani pia alitumia nafasi hiyo kuipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mafia kwa kupata Hati safi kwa Miaka 6 Mfululizo lakini akaitahadharisha kuwa Kupata hati safi ni kwa Mujibu wa Mahesabu waliyotayarisha na kwamba halmashauri iwasaidie Wananchi kupata huduma.

Akigusia juu ya Migogoro ya Ardhi kwenye Halmashauri hiyo, Mhe. Kunenge amesema kuwa ameombea fedha Serikali Kuu ili kisiwa hicho kipimwe na kupangwa na akautaka Uongozi wa Halmshauri hiyo kuwaandaa Wananchi na Mabadiliko Makubwa ya kiuchumi kisiwani hapo.

"Tunataka kisiwa hiki kiwe eneo zuri sana baadhi ya vitu tulivyonavyo tunaongoza Duniani, Mafia ni Lulu” amesema Kunenge.

Kuhusu hoja za ukaguzi, RC Kunenge amemwelekeza Katibu Tawala Mkoa kufuatilia zile zote zilizojirudia na kuwachukulia hatua wote waliosababisha Hoja hizo na akaitaka Halmashauri hiyo kufunga Hoja zote zilizo ndani ya Uwezo wao ifakapo Septemba 30 na kupitia Sheria ndogo na kufanya marekebisho.

Aidha kuhusu Changamoto ya madaktar na wahudumu wa Afya amemwelekeza Mganga Mkuu wa Wilaya kuanza mpango wa Hospital inayotembea (Mobile Clinic) wakati Serikali ikiwa inatafutia Ufumbuzi Changamoto hiyo.

Naye Mwenyekiti wa Halmshauri hiyo Juma Salum Ally amempongeza Mkuu huyo wa Mkoa kwa kuitangaza Mafia, amesema kuwa wamefanikiwa kudhibiti Ukusanyaji wa Mapato ambapo wameongeza kutoka Shilingi Milioni 900 walizokuwa wanakusanya mwaka jana hado Bilioni 1.3 mwaka huu.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.