• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge aiagiza Halmashauri ya rafiji kuepuka kuzalisha hoja za ukaguzi.

Posted on: June 19th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji kuepuka kuzalisha hoja za ukaguzi kwa kuandaa mipango na bajeti kwa kuzingatia vipaumbele vinavyolenga kuwandolea wananchi kero na kuwapatia maendeleo.

Maagizo hayo ameyatoa leo Juni 19, 2023 kwenye kikao maalum cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kilichoketi kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali - CAG kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ambapo wilaya hiyo imepata hati safi.

Amesema kuwa hakuna sababu ya halmashauri kuzalisha hoja iwapo utekelezaji wa shughuli mbalimbali utazingatia na kufuata taratibu zote kwa mujibu wa mipango na bajeti na akaielekeza halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa hoja zote 38 kati 62 zilizopitiwa na kutolewa dosari na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali CAG mwaka wa fedha 2021/2022 zinapatiwa majibu kwa haraka ili ziweze kufungwa.

“Hakikisheni hoja hizi 38 ambazo bado hamjazijibu ikiwa ni pamoja na ya ukusanyaji mapato na uhaba wa wakaguzi wa ndani mnazitolea maelezo haraka ili kupata ufumbuzi wa masuala ambayo yanakwamisha utekelezaji wa shughuli za kuwaletea wanchi maendeleo,“ amesema Kunenge.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Rashid Mchata amewashauri viongozi wa Wilaya hiyo kujipanga, kuhakiki na kuandaa nyaraka na kuzitafutia majibu hoja zote kabla ya mwezi Desemba ili kurahisisha zoezi la ukaguzi wa CAG.

Awali akiwasilisha ripoti ya CAG, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji Michael Gwimile amemuahidi, Mkuu huyo wa Mkoa kushughulikia dosari zote zilizobainika kwenye ripoti hiyo.

Naye Mkaguzi Mkuu wa nje kutoka ofisi ya CAG Mkoa wa Pwani Mary Dibogo ameishauri Halmashauri hiyo kuongeza idadi ya wakaguzi wa ndani kwa ajili ya kushughulikia na kudhibiti mapema dosari ambazo zinaweza kubainishwa na CAG.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.