• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge apongeza Juhudi za Rais Samia katika kuleta maendeleo Pwani.

Posted on: February 23rd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, amepongeza juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan katika kuleta maendeleo mkoani humo, hususan katika sekta za nishati, elimu, na maji.

Akizungumza katika mbio za Samia Marathon zilizofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Mtongani, Mlandizi, Kibaha Vijijini, Kunenge alibainisha kuwa upatikanaji wa umeme vijijini umefikia asilimia 98, huku upatikanaji wa maji ukifikia asilimia 86.

Aidha, shule mpya za msingi 50 na sekondari 42 zimejengwa, pamoja na ukarabati wa mabweni na maboma.

Katika sekta ya Viwanda alisema kuwa mpaka sasa kuna Viwanda vipya 131 kati yake viwanda 78 vikubwa Vimejengwa ndani ya miaka minne.

Katika tukio hilo, Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi (CCM) Taifa, Dogo Mabrouk, alimwakilisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, na kusisitiza kuwa CCM inatekeleza ilani yake kwa kutatua changamoto za wananchi. Alisema Rais Samia ni kielelezo cha uchapakazi na maendeleo, hivyo Watanzania wanapaswa kumuunga mkono kwa ajili ya mafanikio zaidi.

Mbio hizo zilibeba kaulimbiu ya kuhamasisha wananchi kujitokeza kupiga kura katika uchaguzi mkuu ujao mwezi Oktoba. Mabrouk alikumbusha kuwa ingawa wengi hujiandikisha, bado kuna changamoto ya watu kushindwa kujitokeza siku ya kupiga kura, na aliwasihi wananchi kuwa sehemu ya mchakato wa uchaguzi kwa haki na kwa wingi.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kupitia Wazazi mkoani Pwani, Hamoud Jumaa, alisisitiza umoja na mshikamano kuelekea uchaguzi mkuu, akibainisha kuwa umoja ndani ya chama utaleta ushindi kwa CCM. Pia, alihimiza kudumisha amani na utulivu ili kuendeleza mafanikio ya taifa.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani, Josian Kituka, aliwashukuru wadau wote waliofanikisha mbio za Samia Marathon, akieleza kuwa lengo kuu la mbio hizo ni kuhamasisha wananchi kujitokeza kupiga kura.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.