• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge ataka matokeo ya Sensa yatumike kupanga Mipango mizuri ya Maendeleo

Posted on: June 1st, 2023

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge, amewataka wataalamu wa Mkoa huo, kutumia Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, kupanga mipango vizuri ili kutekeleza miradi mbalimbali kulingana na mahitaji ya wananchi.

RC Kunenge ametoa kauli hiyo leo Mei 31, 2023 akizungumza katika mafunzo ya Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi kwa Kamati ya Sensa Mkoa, Sekretarieti ya Mkoa na Viongozi wa Ngazi ya Mkoa wa Pwani yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Chuo cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere mjini Kibaha.

"Tuna mipango mbalimbali, hivyo tuchukue data tulizopata kuziweke katika uhalisia wa mipango yetu," amesema RC Kunenge na kuongeza,

"Nitumie fursa hii kuwaagiza wataalamu wangu kutumia takwimu hizi kuangalia ni wapi tuwekeze nguvu hivyo tuanze kufanya uthibitishaji wa mipango yetu,.

Rc Kunenge ameahidi kufanyia kazi takwimu hizo na kusisitiza kwamba zitawapa dira na mwelekeo mzuri katika kuwahudumia wananchi wa mkoa wa Pwani.

Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi Tanzania Bara Anne Makinda amewashukuru watanzania pamoja na timu yake kufanikisha jukumu la utekelezaji wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022.

Naye Kamisaa wa Sensa Tanzania Zanzibar Balozi Mohamed Haji Hamza amesema jukumu la sasa kwa viongozi ambao wamepata mafunzo hayo ni kusaidia kusambaza matokeo hayo na kuwafikia wananchi wote.

Sambamba na hilo amesema ni kuyaelewa matokeo hayo na namna ya kuyatumia kwa ajili ya mipango ya maendeleo, kwamba lengo ni kujenga jamii yenye kuelewa takwimu za Sensa na kuzitumiwa kwa mipango yao ya maendeleo.

Kwa mujibu wa Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 Mkoa wa Pwani una jumla ya watu 2,024,947 ambapo kati ya hao Wanaume ni 998,616 huku Wanawake wakiwa ni 1,026,331.

Idadi ya watu wenye umri wa kufanya kazi (15-64) ni milioni 1,175,494 sawa na asilimia 58.1, idadi ya wazee wenye umri wa miaka 64 na kuendelea ni 128,432 sawa na asilimia 6.3.

kuhusu idadi ya watoto na vijana ni kwamba kwa vijana wa miaka kati ya 15-25 ni 738,763 sawa na asilimia 36.5 huku watoto wa kati ya miaka 0-14 wakiwa ni 761,525 sawa na asilimia 37.6.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.