• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge azindua Mradi wa Kilimo cha Pamba Rufiji

Posted on: January 13th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe Abubakar Kunenge amezindua Mradi wa kilimo cha Pamba na kupokea matrekta na pikipiki zitazotumika kwenye mradi huo Wilayani Rufiji utakaotekelezwa na Kampuni ya "Rufiji Cotton Ltd.

Akizungumza na Wanachi wa chumbi kwenye hafla hiyo leo Januari 13, 2024 , Mhe Kunenge amewapongeza wawekezaji hao kutoka India kwa uwekezaji huo akisema hana shaka na mwekezaji huyo kwa sababu ni mzoefu kwenye sekta ya Pamba.

Ameeleza kuwa Serikali ipo tayari kumpa ushirikiano mwekezaji na akamtaka atekeleze yote aliyoahidi na kuwa kupitia uwekezaji huo vijana watapata ajira, ujuzi na kodi kwa serikali.

"Kilimo ndio kipaumbele kwa Mkoa wa Pwani lakini bado hakijafanya vizuri, hivyo nnawapongeza wakazi wa Chumbi kwa kuwezesha uwekezaji huu na pia nnaipongeza Wilaya ya Rufiji kwa kuendelea kuwapokea wawekezaji, kwa sasa wilaya hii ina wawekezaji wakubwa wa Kilimo cha Sukari na sasa Kilimo cha Pamba na niwaase kuzitumia fursa hizi mlizopata.

Kwenye uzinduzi huo, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pamba Bw. Wille Mtunga ameeleza kuwa uzinduzi wa mradi huo ni matokeo ya ziara ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan nchini India. Ameeleza kuwa wataalam wa Bodi hiyo wamepita katika vijiji 24 wilayani Rufiji kufundisha juu ya kilimo bora cha pamba na kuwa ili kuwa na kilimo bora, wameleta timu ya ushindi ambao ni maafisa ugani 24 watakao hudumu kwenye vijiji hivyo 24 na kuwa mpaka sasa wamesajili wakulima wenye jumla ya ekari 3012 wilayani humo na kafafanua kuwa ifikapo Jumatatu Januari 15, 2024 watapeleka mbegu za pamba, viwatilifu, mabomba ya kupulizia mazao na vyote vitagawiwa kwa wakulima bila malipo.

Kwa upande wake Balozi wa zao la Pamba nchini Mhe. Aggrey Mwanri ametuma salaam kwa Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan za pongezi kwa kuvutia uwekezaji katika sekta ya Pamba. Kazi yangu kama balozi ni kufanya pamba ipendeke kwa wananchi wote, tumechukua takwimu za wananchi wote wa Rufiji waliotayari kulima Pamba kwani kilo zinazozalishwa wilayani Rufiji ni laki moja na kiwanda kitakachojengwa kitahitaji kilo laki tano kwahiyo Halmshauri hii ikilima pamba vizuri itapata ruzuku," amefafanua Mwanri.

Balozi huyo wa Pamba amehamasisha vijana wote kulima zao hilo na akawataka maafisa ugani 24 walioajiriwa kuhakikisha wanafanya kazi iliyokusudiwa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha "Rufiji Cotton Ltd." Bw Hassan Kinje ameeleza kuwa wamkwenda kuwekeza kwenye kilimo cha Pamba Rufiji kwa sababu ya Mazingira mazuri ya uwekezaji na akabainisha kuwa kampuni hiyo itatoa uwezeshaji wa huduma bure ya matrekta kwa ajili ya kilimo.

Aidha ameeleza kuwa wameajiri maafisa ugani 24 na kutoa pikipiki ambazo zitatumika kutoa elimu kwa wakulima na kwamba wanategemea kujenga kiwanda cha kuchambua Pamba na kiwanda cha nguo na akapongeza ushirikiano mkubwa walioupata kutoka kwa uongozi wa Mkoa katika kufanikisha uwekezaji huo.

Diwani kata ya Chumbi Mhe. Ally Athuman Nguyu amepongeza Wananchi kujitolea ekari 6000 kwa ajili ya kilimo cha Pamba na ujenzi wa kiwanda cha kuchakata pamba na akahamasisha wananchi kulima pamba kwa wingi kwa kuwa mwekezaji anahitaji pamba nyingi zaidi hivyo wananchi wote walime ili kuweza kulisha kiwanda hicho.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.