• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge: Hali ni nzuri Uwingi wa Maji, usafi mazingira Mto Ruvu

Posted on: November 5th, 2023

Mkuu wa mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ameeleza kuridhishwa na namna bonde la Mto Ruvu limelindwa kwa kuhakikisha hakuna uharibifu katika vyanzo vya maji vinavyoweza kusababishwa na shughuli za kibinadamu kama vile ufugaji na kilimo.

Kunenge ametoa kauli hiyo leo Novemba 4, 2023 kwenye ziara ya kukagua na kuangalia hali ya utunzaji wa bonde la Ruvu ambalo lina vituo viwili vya kuzalisha maji, Ruvu juu na chini mkoani Pwani.

Katika ziara hiyo, RC Kunenge aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka ambaye alimwakilisha Mkuu wa mkoa wa Morogoro Adam Malima, timu ya wataalam kutoka ofisi ya bonde la otiWami - Ruvu, Mamlaka ya Maji safi na Salama Dar es Salaam DAWASA, na timu ya waandishi wa habari ambao wamefika na kujionea kazi nzuri iliyofanywa ya utunzaji wa bonde hilo.

Amesema ziara hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa jukumu la kusimamia bonde hilo ili kuwa na kiwango kikubwa cha maji ambacho kitasaidia upatikanaji wa uhakika wa maji kwa wananchi wa mikoa ya Pwani na Dar es Salaam pamoja na usafi wa kutoa taka kwenye bonde hilo ili maji yanayopatikana yawe safi na salama.

“Baada ya kubaini bonde hili lina upungufu mkubwa wa maji kwa miaka ya nyuma, tulikubaliana sisi wakuu wa mikoa ya Morogoro, Pwani na Dar es Salaam kuweka mikakati itakayowezesha maji kupatikana kwa wingi, mikakati hiyo ni pamoja na kuhamasisha zoezi la upandaji miti kuzunguka bonde hilo, kuzuia shughuli za kibinadamu ikiwemo uchepushaji wa maji kwa ajili ya kilimo na ufugaji iliyokuwa inafanywa na baadhi ya wananchi,” amesema Kunenge.

Ameongeza kuwa baada ya kazi hiyo ambayo iliwahusisha wataalam wa bonde na DAWASA, muitikio wa utunzaji umekuwa mzuri kwani shughuli za uchafuzi wa mazingira zimepungua.

Katika hatua nyingine Kunenge amewataka wananchi kuchukua tahadhari juu ya mvua zinazoendelea kunyesha kama vile kuhama kwenye mabonde na maeneo yaliyo jirani na mito ili kuwa salama dhidi ya mafuriko yanayoweza kutokea.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Adam Malima, Mkuu wa wilaya ya Kilosa, Shaka Hamdu Shaka, amesema wanatekeleza maagizo ya Rais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan kuhusu utunzaji wa bonde la Wami - Ruvu ambalo mwaka 2022 lilikuwa na uhaba wa maji.

Amesema kwa pamoja viongozi wa mikoa mitatu inayonufaika na bonde hilo wataendelea kufanya ukaguzi wa mara kwa mara ili kudhibiti uharibifu wa mazingira.

Mkurugenzi wa Bonde la Wami - Ruvu, Elibariki amesema mvua za vuli zinazoendelea kunyesha mwaka huu zimesaidia kuongeza maji katika bonde hilo kutoka asilimia 29 ya mwaka jana na kufikia 69.

Amesema hali hiyo inatokana na utunzaji wa mazingira katila vyanzo vya mito inayotiririsha maji yake katika bonde hilo ambalo safu zake zinaanzia kwenye milima ya Uluguru.

Ameongeza kuwa kwa sasa wana uhakika wa maji ya kusambaza kwa wananchi wa mikoa ya Pwani na Dar es Salaam na kwamba Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini TMA imewahakikishia kutakuwa na mvua nyingi ambazo zitasaidia kuongeza wingi wa maji.

S

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.