• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Kunenge,Makalla Wakagua Hali ya Maji Ruvu

Posted on: July 15th, 2022

Wakuu wa Mikoa ya Pwani na Dar es Salaam leo Julai 15, 2022 wametembelea mitambo ya Ruvu Juu na chini inayosukuma maji kupeleka Maeneo mbalimbali ya Mikoa hiyo.

Akiongelea hali ya upatikanaji maji Katika mto Ruvu ambacho ndicho chanzo kikuu kwa Mkoa wa PWANI na Dar es Salaam, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge amewahakikishia Wakazi wa Mkoa huo kuwa wameridhishwa na hali ya upatikanaji wa huduma.

Amesema kuwa pamoja na hali ya kiangazi kilichopo sasa, DAWASA imechukua hatua stahiki za kukabiliana na tatizo la uhaba wa maji msimu wa kiangazi ikiwemo Ujenzi wa Mabwawa ya kutunza Maji.

RC kunenge alihamasiha wanachi kuchukua tahadhari mapema akisema “Tuchukue tahadhari mapema ili kudhibiti upotevu wa maji na tusijikute tunapambana na hali ya mwaka Jana.”

Amesema kuwa hali ya Kina cha maji waliyoikuta kwenye mitambo ya Ruvu juu ni mita 16.5 na Ruvu Chini Mita 4.2 ambapo kwa mujibu wa DAWASA kiwango hicho Kwa sasa kinaweza kutuvusha salama kipindi cha kiangazi.

RC Kunenge amewataka wale wote wenye vibali vya kutumia maji hayo watumie vizuri kwa mujibu wa Vibali vyao na wale ambao wanachepusha maji bila ya vibali waache mara moja ili wasisababishe athari kubwa, na akatoa wito kwa waumini na viongozi wa Dini mbalimbali kufanya maombi na Dua za kuombea mvua za Vuli zinyeshe na bila kusababisha majanga yoyote yale.

Pamoja na hayo kunenge amemshukuru na kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa jitihada za dhati anazofanya kuboresha sekta ya Maji kupitia miradi Mikubwa na midogo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla ameielekeza Kamati ya Ulinzi na usalama na Mamlaka ya Bonde la Wami/Ruvu kufanya Operesheni za Mara kwa mara na kuwachukulia hatua watu watakaobainika kuchepusha maji bila Vibali.

Naye Mtendaji Mkuu wa DAWASA Eng. Cyprian Luhemeja amesema Mamlaka hiyo inaendelea kufanya kila jitihada za kuhakikisha kiasi Cha Maji kilichopo kinalindwa na kudhibiti upotevu na akawataka Wananchi kutunza na kulinda Vyanzo vya Maji ili kuwepo na upatikanaji wa maji ya uhakika.

Ziara hiyo pia iliwashirikisha viongozi mbalimbali Katika Mikoa hiyo wakiwemo Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na kamati za ulinzi na usalama.

Mwaka Jana maeneo mengi ya Jiji la Dar es salaam yalikumbwa na tatizo la uhaba wa maji Kutokana na ukame uliosababishwa na kutokunyesha kwa mvua za Vuli.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.