• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC NDIKILO AAGIZA KUKAMATWA MARA MOJA WALE WALIOWAPA MIMBA WANAFUNZI 20

Posted on: December 8th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo ameliagiza Jeshi la Polisi Mkoani Pwani, kuwasaka wale wote waliohusika kuwapa mimba wanafunzi 20 waliokosa kuhitimu elimu ya msingi mwaka huu.

Amesema, wanaume wanaowatongoza watoto wa kike waliopo shule, wanatakiwa kushtakiwa kwa mujibu wa sheria na kufungwa miaka 30 jela.

Akifungua kikao cha bodi cha matokeo ya wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2018, Mhandisi Ndikilo alisema, Jeshi la Polisi lianze na wahusika hao kwakuwa wanajulikana.

Alieleza hataki kusikia mwalimu mkuu ama mzazi anakaa kumalizana na watuhumiwa wanaohusika kuwapa mimba watoto bali wahakikishe wanatoa ushirikiano ili wachukuliwe hatua stahiki. Aliwaasa wanafunzi wa kike kuacha kushawishiwa kwa chipsi, simu na badala yake wajikite kwenye elimu ambayo ni msingi wa maisha yao.

“Naagiza Jeshi la Polisi kuwakamata watu hao waliowatia mimba wanafunzi wakashindwa kufanya mitihani yao ya kumaliza darasa la saba mwaka huu,”

“Mifataki hii,inashindwa kuwafuata saizi zao wanaenda kuwarubuni watoto wa shule, wakashindane kwa hoja na wanawake walio saizi zao, sio kushindana kwa hoja ya chipsi,kuku,au simu” alisema Mhandisi Ndikilo.

Aliwapongeza walimu, Maafisa Elimu na waratibu wa Elimu Mkoani Pwani kwa kuongeza jitihada na kusababisha ufaulu kimkoa  kwa mwaka huu kupanda na kufikia asilimia 66.9 na kusema kuwa ni hatua nzuri . Alibainisha, ufaulu umeongezeka katika halmashauri ikiwa ni sanjari na Kibiti 54.02 na Rufiji 52.94 licha ya Wilaya hizo kukumbwa na hali ya kiuhalifu kwenye kipindi hicho.

Katibu Tawala wa Mkoa Ndg. Zuberi Samataba ambaye alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho alielezea, watahakikisha wahusika wanakamatwa na kufikishwa mahakamani. Aidha alisema kuwa, kila Halmashauri inawajibu kutafuta sababu zilizopelekea kufanya vibaya kwa shule hizo kumi ili kupata ufumbuzi wa haraka.

Samataba aliwataka walimu kutimiza wajibu wao na kuacha kutoroka nyakati za kazi na kwenda mijini kufanya mambo mengine “Walimu na wazazi washirikiane na Idara ya Elimu Wilaya na Mkoa kukabiliana na changamoto zinazosababisha taaluma kushuka ili kuhakikisha matokeo ya mwaka ujao yanapanda zaidi ya sasa” .

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu Ndg. Abdul Maulid alisema, wanafunzi 101 sawa na asilimia 0.37 hawakufanya mtihani kwasababu mbalimbali ikiwemo mimba. Wanafunzi wengine 60 ni watoro, vifo sita ,ugonjwa 12 na sababu nyingine.

Hata hivyo, Maulid alisema hali ya matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu Mkoani Pwani, imepanda kutoka asilimia 62.57 mwaka 2016 hadi kufikia asilimia 66.9 mwaka 2017 sawa na ongezeko la asilimia 4.33.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.