• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC Ndikilo ashiriki mnada wa kwanza wa Korosho Pwani

Posted on: November 28th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo ameshiriki na kushuhudia mnada wa kwanza wa Korosho kwa msimu wa mauzo wa 2019  Mkoani hapa ambapo jumla ya kilo 156,257 kwa Daraja la kwanza na la Pili zimeuzwa.

Katika mnada huo, Korosho Daraja la Kwanza ambazo ni kilo  46,781 zimeuzwa kwa bei ya shilingi 2,571 kwa kilo na kampuni iliyozinunua ni Alpher Choice Ltd. na Korosho daraja la Pili kilo 109,476  zimeuzwa kwa bei ya shilingi 2,300 na zimenunuliwa na kampuni CDJKL Nuts Ltd.

Akifungua mnada huo Mhandisi Ndikilo amewataka wanunuzi wote kuhakikisha kuwa wanalipa fedha hizo si zaidi ya siku kumi na kuichukua Korosho yao.

Katika hotuba yake ya ufunguzi wa mnada huo, Mhandisi Ndikilo amewataka wakulima wa Korosho Mkoani Pwani kuhakikisha wanatunza mikorosho yao kwa kuipalilia ili waweze kuzalisha Korosho zilizo na ubora mzuri na akaonya tabia ya baadhi ya watu kuweka mchanga na mawe kwenye magunia ya korosho kwani kufanya hivyo ni udanganyifu unaoliharibia zao hilo soko na unauletea Mkoa na Taifa sifa mbaya.

Awali Mhandisi Ndikilo alizungumza na wadau wa zao la Korosho kwenye kikao maalum kilichojadili mwenendo wa uzalishaji zao la Korosho changamoto za kuchelewa kufanyika mnada wa zao hilo kutokana na hali ya hewa kufuatia mvua nyingi kunyesha kwa Zaidi ya miezi mitatu.

“Baadhi ya AMCOS hazikuchambua na kupanga korosho katika madaraja kutokana na viwango vya ubora, hali iliyosababisha baadhi ya AMCOS kurudisha korosho kwa uchambuzi Zaidi na kufanya marekebisho yanayohitajika: alisema Mhandisi Ndikilo.

Mhandisi Ndikilo alifafanua kuwa hali hiyo ilisababisha uongozi wa Mkoa kukaa na viongozi wa chama kikuu cha CORECU na kufikia maamuzi kuwa AMCOS sasa zikusanye korosho kwenye maghala yao lakini wasisafirishe kwenda ghala kuu hadi uchambuzi uwe umefanyika.

Kwenye mkutano huo, Mhandisi Ndikilo amekemea tabia ya baadhi ya viongozi wa AMCOS kutumia Stakabadhi bandia kwa lengo la kuwadhulumu Wakulima na akaonya kuwa AMCOS zitakazobainika kuwaibia wakulima zitavunjwa zote na viongozi wao watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Mhe. Ndikilo alisema kuwa hali ya mapokezi ya korosho kwenye maghala makuu bado sio nzuri.

Pia alisema kuwa zaidi ya kilo milioni 20 zinatarahiwa kukusanywa kutoka kwa wakulima kwa msimu wa mauzo ya mwaka huu wa 2019 na kwamba korosho nyingi zipo kwenye maghala ya AMCOS ambako zinaendelea kufanyiwa tathmini ya ubora na nyingine zimekaguluwa na kubainika kuwa na ubora hafifu ambao nje ya madaraja rasmi yanayotambuliwa na sheria ya Bodi ya korosho.

“Korosho zisizo na ubora ziendelee kuhifadhiwa hadi wadau watakapokaa na kuamua hatma ya Korosho hizo” aliongeza Mhandisi Ndikilo.

Kikao hicho kilifanyika Wilayani Mkuranga na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa korosho wakiwemo Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, wakulima wa zao la Korosha, wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa pamoja na wadau kutoka Bodi ya Korosho.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.