• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

RC NDIKILO AWASIMAMISHA KAZI WATUMISHI WAWILI WA KAMPUNI INAYOJENGA RELI YA STANDARD GAUGE

Posted on: October 6th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Mhandisi Evarist W. Ndikilo amewasimamisha watumishi wawili wa kampuni ya ujenzi ya Yapi Merkezi ya nchini Uturuki inayojenga reli ya Standard Gauge kutoka Dar es Salaam - Morogoro kwa tuhuma za rushwa ya ajira.

Aidha ameagiza watumishi hao wasimamishwe kupisha uchunguzi huku akitoa siku saba kwa vyombo vya dola kufuatilia suala hilo.

Mhe. Ndikilo, aliyasema hayo wakati alipotembelea ujenzi wa mradi huo kwenye kijiji cha Soga wilayani Kibaha.

alieleza kuwa endapo ikibainika wamehusika na vitendo hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Aliwataja watumishi hao ambao walikuwa wakilalamikiwa na wananchi waliokuwa wakienda kuomba kazi kuwa walikuwa wakiomba rushwa ni pamoja na Nelson ambae ametambulika kwa jina moja Afisa mwajiri(HRO) kwenye kampuni hiyo.

Mwingine ni Torong’ong’o ambaye ni dereva wa moja ya viongozi wa kampuni hiyo ambao hawakuhudhuria hata kwenye mkutano huo.

Awali Mhandisi Ndikilo alipokelewa kwa mabango na watu waliokuwa nje ya kampuni hiyo wakilalamika kunyimwa ajira za udereva na uendeshaji wa mitambo wakidai kuwa ajira zinatolewa kwa njia ya rushwa.

“Tunanyimwa ajira hasa tunaotoka maeneo ya Kibaha na Mkoa wa Pwani kwa ujumla na wanaoajiriwa ni watu wa nje ya Mkoa” walisema.

Mhandisi Ndikilo, alielezea kwamba alikuwa pia akipelekewa malalamiko ofisini kwake ambapo baadhi ya madereva waliandika majina yao na kuambatanisha vyeti vyao na uzoefu wao wa kazi lakini hawakupata ajira.

“Malalamiko yamekuwa ni mengi sana na wanaolalamika wanasema wamenyimwa ajira wengi ni wa hapa Kibaha na Mkoa wa Pwani ambao walipaswa kunufaika na mradi huu kwani kila eneo lenye mradi lazima wahusika wa eneo wapewe kipaumbele, inadaiwa walioajiriwa, wenyeji hata 100 hawafiki katia ya 390 ya walioajiriwa,” alisema Ndikilo.p

Kwa upande wake  Meneja wa mradi huo ulio chini ya Reli Assets Holding Company (RAHCO), Mhandisi Maizo Mgedzi alisema kuwa watahakikisha wanalifuatilia suala hilo ili kupisha uchunguzi lengo likiwa ni kuhakikisha hakuna malalamiko kwa wananchi wanaozunguka eneo la mradi huo.

Naye mwakilishi wa kampuni ya Yapi Merkezi  Mhandisi Mert Oz alisema, endapo watabaini wapo walioingizwa kwenye ajira kinyume cha utaratibu, hawatasita kuwaondoa.

Mhandisi Oz alisema, wanafuata taratibu za ajira na wanategemea kuletewa wafanyakazi kwa utaratibu wa nchi na kufuata sheria za ajira.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.