• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Serikali yaagiza ukaguzi kianda cha Vitendanishi Pwani

Posted on: September 23rd, 2023

Serikali imeiagiza Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba TMDA na Bohari kuu ya Dawa MSD, kufanya ukaguzi katika kiwanda cha kuzalisha vitendanishi kwa ajili ya kupima sampuli za damu kilichopo Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani ili kianze uzalishaji.

Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel amezindua kiwanda hicho kijulikanacho kwa jina la Action Medeor kilichopo Kibaha mkoani Pwani na akasema kiwanda hicho kitapunguza gharama za ununuzi wa vitendanishi walizokuwa wakinunua kwa shilingi 300,000 hadi 400,000 na sasa uwepo wa kiwanda hicho utapunguza gharama hizo hadi sh. 80,000.

Kutokana na hilo amemuagiza Mkurugenzi wa TMDA na MSD kufika kiwandani hapo ndani ya wiki mbili ili kukagua na kutoa kibali cha kuanza uzalishaji wa vitendanishi.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya Zanzibar, Hassan Hafidh amesema umefika wakati kwa serikali kuyafuta makampuni ambayo yanauza bidhaa hiyo kwa gharama kubwa zinazowashinda wananchi kumudu.

“Nimefurahishwa na uwekezaji mkubwa wa kiwanda hiki na niseme tu kuwa gharama za bidhaa hii kiwandani hapa wanauza kwa bei rafiki kabisa, sasa nakwenda Zanzibar nitafuta viwanda vyote vinavyouza vitendanishi kwa gharama kubwa,” amesema Naibu Waziri Hafidh.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Actiob Medeor, Christoph Bonsmann, amesema kiwanda hicho kitapunguza gharama za matibabu nchini Tanzania kwa zaidi ya asilimia 200.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Nickson Saimon amesema uwepo wa kiwanda hicho utaipunguzia mzigo serikali katika uendeshaji wa shughuli zake za matibabu.

Amesema serikali inatumia gharama kubwa katika kuhakikisha huduma za matibabu nchini zinapatikana kwa urahisi hivyo uwepo wa kiwanda hicho ni sehemu ya kuunga mkono jitihada hizo na kwamba wanafurahi mkoa wa Pwani kuwa sehemu ya uwekezaji wa huduma za matibabu.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.