• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Tanzania Inajitosheleza Uwekezaji sekta ya Viwanda -Waziri Mkuu Majaliwa

Posted on: August 19th, 2020

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amesema kuwa Tanzania imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji wa miradi mbalimbali.

Mhe. Majaliwa aliyasema hayo alipotembelea kiwanda cha Bagamoyo Sugar Co. Ltd, kilichopo Makurunge Wilayani Bagamoyo kujionea utekelezaji wa mradi huo ambao Unatarajia kugharimu Dola za kimarekani milioni 100.

Akiwa katika eneo la mradi huo, Mhe. Majaliwa pamoja na kuzunguka kukagua namna utekelezaji wa mradi huo wa shamba la miwa na ujenzi wa kiwanda cha sukari unavyotekelezwa, amezugumzia jinsi Tanzania ilivyoweka mazingira mazuri ya uwekezaji hivyo kupelekea kupiga hatua kubwa katika sekta ya viwanda.

Mhe.Majaliwa ametanabahisha kuwa, Serikali ya Awamu ya tano iliamua kuinua uchumi wa ndani kwa kuimarisha uwekezaji wa sekta ya viwanda, ambapo matokeo yameshaanza kuonekana kwani sasa Nchi ya Tanzania imefikia uchumi wa kati kabla ya malengo iliyojiwekea kufikia ngazi hiyo ifikapo Mwaka 2025 na imetokana na maboresho makubwa ya mifumo ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa Sekta ya viwanda kwa kukaribisha wawekezaji wa ndani na wa nje.

“Maboresho haya makubwa ya mifumo yetu ya kiuchumi kupitia uwekezaji wa sekta ya viwanda yamefanikiwa kwakuwa Tanzania tumejitosheleza kuendesha sekta hii ya viwanda, tuna Amani inayofanya Tanzania kuwa mahali salama pa uwekezaji, tuna malighafi zinazotokana na ardhi nzuri tuliyonayo, wataalam wazoefu wa kutosha, miundo mbinu ya barabara, reli, maji na umeme ambayo inaendelea kuboreshwa kila uchao ambavyo vyote vinaifanya Tanzania kujitosheleza kiuwekezaji wa Sekta ya Viwanda” Amesema Mhe. Majaliwa.

Waziri Mkuu huyo ameongeza Kusekwa kuwa ili Sekta ya viwanda iendelee kufanya vizuri ni lazima eneo la malighafi liwekewe msisitizo. “Tunajua tuna malighafi za kilimo ambazo zinatumika viwandani, tuna malighafi za madini, maliasili na aina karibu zote za malighafi zinazotumika viwandani Tanzania zinapatikana, hivyo sisi Tanzania ni matajiri kwasababu hizi malighafi zote tunazo na tunaendelea kuwakaribisha wawekezaji wa ndani na wa nje kuja kuwekeza Tanzania kwani tunajitosheleza” Amesema Mhe. Majaliwa

Waziri Mkuu amefanya ziara maalum kutembelea kiwanda cha sukari cha Bagamoyo Sugar Company limited kilichopo eneo la Makurunge Wilayani Bagamoyo, kujionea uendelevu wa utekelezaji wa uwekezaji wa kiwanda hicho ambacho kinajengwa baada ya Serikali kuipatia Bakhresa group of companies eneo lenye ukubwa wa hekta 10,000 ili wafanye kilimo cha miwa na kujenga kiwanda cha sukari, uwekezaji utakaogharimu jumla ya Dola Milioni 100, huku Benki ya Wakulima Nchini (TADB) tayari ikiwa imeshatoa mkopo wa Dola Milioni 6.5 kusaidia uwekezaji huo, hivyo kuifanya Serikali kuwa mdau mkubwa katika uwekezaji huo ambao utaiondoa Tanzania katika upungufu wa takribani Tani 70,000 za sukari zinazohitajika kwa matumizi Nchini.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.