• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

Trilion 6 zatekeleza Miradi Pwani

Posted on: November 3rd, 2023

Mkuu wa mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema katika kipindi cha miaka mitatu mkoa huo umepokea kiasi cha sh. Trilion 1.19 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Amesema fedha hizo zimetumika kutekeleza miradi ya afya, elimu, maji na miundombinu na hivyo kupunguza vikwazo vilivyokuwa vinakwamisha maendeleo kwa wananchi.

Amebainisha hayo leo Novemba 3, 2023 wakati akizungumza katika mkutano na vyombo vya habari uliofanyika mjini Kibaha ulioandaliwa na ofisi yake kwa kushirikiana na ofisi ya msemaji mkuu wa serikali na kuhusisha viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa huo Abubakar Kunenge, kamati ya siasa ya CCM mkoa na Wilaya ya Kibaha, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa halmashauri, wakuu wa sehemu na vitengo Mkoa pamoja na wakuu wa taasisi za serikali ambao walielezea miradi iliyotekelezwa.

Kuhusu Miradi ya miundombinu ya barabara, amesema serikali ipo mbioni kuanza ujenzi wa upanuzi wa barabara kuanzia Dar es Salaam - Chalinze - Morogoro ambayo itakwenda kuondoa msongamano .

Aidha Kunenge amefafanua kuwa ujenzi wa barabara ya Chalinze-Utete ambayo itafungua milango ya kiuchumi na maendeleo katika maeneo hayo.

Katika mkutano huo, Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi, amesema viongozi wa Serikali wanatakiwa kuelezea miradi waliyoitekeleza ili kuondoa pengo kati ya wanachokiona Wananchi na kinachofanywa.

Ili kukabiliana na hali hiyo, amesema ni jukumu la viongozi na watendaji kueleza makubwa yanayofanywa na Serikali kwa wananchi kupitia mikutano mbalimbali.

Matinyi amesema, Serikali imekuwa ikipeleka fedha nyingi za miradi ya Maendeleo ya wananchi lakini hawaelezwi mchanganuo wa namna inavyotekelezwa ili kujua namna uongozi wao unavyowasaidia.

"Viongozi wa mikoa wanatakiwa kusimamia fedha za utekelezaji wa miradi hiyo ili iweze kuleta matokeo chanya kwa wananchi sambamba na kuwashirikisha kwa kila hatua kwenye maeneo husika," amesema.

Akielezea kuhusu mkutano huo amesema ni moja ya mpango uliozinduliwa hivi karibuni Jijini Dodoma kuwezesha viongozi kuelezea utekelezaji wa miradi mbalimbali iliyofanywa na Serikaii kwa kipindi cha miaka mitatu na itaendelea katika mikoa yote 26 ya Tanzania bara ili taarifa za Serikali ziwafikie wananchi.

Katika mkutano huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Hemed Magaro ameishukuru Serikali kwa namna ilivyotoa fedha za miradi ambayo imekwenda kutatua vikwazo kwa wananchi hususani katika eneo la delta.

"Awali wananchi wa Mbwera walikuwa wanasafiri km 90 kwenda kupata huduma za afya na wakati wa mvua walikuwa hawawezi kusafiri, hivyo ujenzi wa kituo cha afya katika eneo lao umeondoa tatizo lililokuwa linawakabili," ameeleza.

Kadhalika Kaimu Mkurugenzi wa wilaya ya Kisarawe, Deogratius Lukomanya, amesema kipindi cha miaka mitatu, Idara ya Elimu Msingi imefanikiwa kufikisha madarasa 616 kutoka 375 yaliyokuwepo na imejenga matundu 200 ya vyoo.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.

  • Situs Toto
  • Situs Slot Gacor
  • AXL777
  • Situs Toto
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • DORA77
  • DORA77
  • DORA77
  • Toto Togel
  • Situs Toto
  • AXL777
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Toto Slot Gacor
  • Toto Slot
  • Toto Slot
  • DORA77
  • KOI200
  • KOI200
  • SILVAWIN
  • AXL777
  • YAMITOTO
  • NABITOTO
  • YAMITOTO
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200