• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Waandishi wa habari amkoa wa Pwani wajengewe uwezo utekelezaji wa mradi wa Shule Bora

Posted on: December 8th, 2022

Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani Zuwena Omari amewaasa waandishi wa habari kutumia nguvu ya kalamu zao kuandika taarifa za mradi wa Shule Bora unaolenga kuweka mikakati sahihi na kutafuta suluhisho ili kuhakikisha Watoto wa makundi maalum, wa kike na wa kiume wanapata elimu iliyo kwenye mazingira bora.

Rai hiyo ameitoa leo Disemba 8, 2022 wakati akifungua mafunzo ya uhamasishaji wa mradi wa Shule Bora kwa waandishi wa habari na wasimamizi wa vyombo vya habari mkoani humo ambapo pia aliwaasa kuendelea kuimarisha mahusiano baina ya Serikali na vyombo vya habari ili mradi huo ulete tija.

"Hakuna asiyejua nguvu ya kalamu za waandishi wa habari, kwa kuandika taarifa zinazoaminika kwenye kampeni za maendeleo nchini, sisi Kama mkoa tutaimarisha mahusiano na vyombo vya habari ili kuhakikisha mradi unaleta mafanikio "alifafanua Zuwena.

Akielezea mradi huo, Zuwena alibainisha kuwa umefadhiliwa na mfuko wa UKaid unaolenga kuunga mkono uboreshaji wa elimu msingi Tanzania kwa miaka sita katika Halmashauri 67 mikoa 9 yaTanga, Pwani, Dodoma, Singida, Kigoma, Katavi ,Simiyu, Mara na Rukwa na itahusisha watoto milioni 3.8 katika maeneo hayo ya utekelezaji.

"Utekelezaji wa mradi umelenga kuboresha ufundishaji kwa walimu, kuboresha elimu awali na ya msingi iliyo jumuishi kwa makundi ya watoto wenye mahitaji maalum, kuboresha ujifunzaji kwa wanafunzi pamoja na kuboresha mfumo wa usimamizi wa sekta ya elimu katika kuhakikisha kila kiongozi anawajibika ipasavyo kwa nafasi yake ili kufikia azma iliyokusudiwa" alisema Katibu Tawala huyo.

Kwa upande wake Afisa elimu mkoa wa Pwani Sara Mlaki alieleza kuwa mradi wa Shule Bora ulizinduliwa Kitaifa na Kimataifa mwaka 2021 katika shule ya msingi Mkoani kwenye Halmashauri ya Kibaha Mji mkoani Pwani.

Sara lifafanua kuwa kwa sasa zipo kazi zinazoendelea kufanywa kulingana na matakwa ya mradi ikiwa ni sanjari na uboreshaji wa aufundishaji darasa madarasa ya awali, uimarisha usimamizi wa shule na elimu katika Mamlaka za Serikali za mitaa ambapo wameshaanza kuona matokeo chanya kwani ufaulu umepanda.

Sara alieleza mradi huo unakusudia kuondoa changamoto zinazowakabili watoto kushindwa kusoma, kuandika na kuhesabu, kuondoa tatizo la utoro na kutowapa fursa watoto wenye mahitaji maalumu katika kuendelea na elimu ya sekondari.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa habari Mkoani Pwani, Ally Hengo alishukuru kundi la waandishi kutambuliwa na kushirikishwa kwenye utekelezaji wa mradi huo na akaeleza kuwa wanashukuru waandishi kuachiwa mlango wazi kupata taarifa ama kupewa ufafanuzi juu ya masuala ya elimu kupitia maafisa habari kwani changamoto kubwa wanayoipata ni kukosa taarifa kwa wakati.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.