• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Wafanyakazi Mkoani Pwani Wajitokeza Kumpongeza Mhe. Rais Magufuli

Posted on: January 13th, 2019

Watumishi mbalimbali kutoka  Mkoni  wa Pwani wameungana kwa pamoja na kufanya maandamano ya amani yaliyolenga kumpongeza Mhe. Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, kwa kuweza kurejesha kikokotoo cha zamani cha mafao ya Wastaafu.

Maandamano hayo yamefanyika mwishoni mwa wiki hii katika viwanja vya Shirika la elimu Kibaha,  ambapo yalijumuisha wafanyakazi wote wa Serikali , mashirika ya umma pamoja na Sekta binafsi,  maandamano hayo yalipokelwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Mhandisi Evarist Ndikilo, ambaye ndie alikuwa mgeni rasmi.

Akisoma hotuna kwa niaba ya wafanyakazi , mratibu wa Shirikisho la vyama vya Wafanyakazi [TUCTA] Mkoa wa Pwani , Kassim Matewele alisema pamoja  na nia njema ya Serikali  ya kuunganisha  mifuko hiyo ya jamii yapo mambo ambayo wanachama wa mifuko hiyo hawakuridhishwa nayo, ikiwa pamoja na {fomula}  yaani kikokotoo kilichotumika ambacho kilipunguza mafao ya watumishi kwa asilimia 62.9%.

Aidha Matewele alisema kuwa Wafanyakazi wamepokea kwa furaha na wamekuwa na faraja kubwa na maamuzi ya Mhe. Rais na kusema kuwa uamuzi huu ni wa kiungwana na  umeonesha kuwajali wafanyazi hasa wastaafu waliotumikiaTaifa hili.

“ Tunampongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kuamua kurudisha kikokotoo kilichokuwa kikitumika awali kwa mifuko yote.Kupitia maandamano haya sisi wafanyakazi wa Mkoa wa Pwani tunampongeza na tunamshukuru sana Mhe. Rais kwa uamuzi wake wa busara kwa kujali maslahi ya wafanyakazi na Taifa kwa ujumla.

Matewele aliendelea kusema kuwa pamoja na uamuzi huo wa Serikali, pia wanayo  maombi kadhaa kwa Mhe. Rais ikiwa ni  pamoja na kuomba kupandishiwa mishahara, madaraja , vyeo na ulipaji wa malimbikio pamoja na urekebishaji wa mafao kwa baadhi ya mifuko ya jamii kama GEPF, PPF, NSSF ambapo wameomba mifuko hiyo wapandishe nao wafike asilimia 50%.

Akionge a mara baada ya kupokea hotuna ya wafanyakazi , Mkuu wa Mkoa wa Pwani , Mhandisi Evarist Ndikilo  nae ameungana na wafanyakazi hao katika kumpongeza Mhe Rais kwa namna  alivyotolea Tamko suala hilo.

Mhandisi Ndikilo alisema kuwa  alichokifanya Mhe. Rais ni jambo kubwa na la neema na heshima kwa wafanyakazi.

“ Serikali ya awamu ya Tano chini ya Uongozi wa Mhe. Rais Dkt John Pombe Magufuli  ni sikivu sana na inawajali wanyonge na inachukua hatua stahiki kwa wakati na muda muafaka alisema Mhandisi Ndikilo.

Aidha amewataka watumishi wote kwenda kufanya kazi kama kauli mbiu ya hapa kazi tu inavyohamasisha.

“Kila mtu kwa  kwa nafasi yake aende akawajibike, na sisi Serikali tunahidi kuendelea kutimiza wajibu wetu kama ambavyo mmetupa dhamana ya kuwaongoza “ alibainisha Mhandisi Ndikilo.

Sambamba na hilo Mhandisi Ndikilo  amewapongeza watumiashi wa Mkoa wa Pwani  kwa kuwa na nidhamu  katika kazi ambapo wamekuwa wakiwahudumia wananchi vizuri na kuondoa malalmiko kwa wananchi.

Katika Hatua nyingine Mhandisi Ndikilo amekemea vikali vitendo vinavyofanywa  na wamiliki na waajiri wa viwanda wanaowafanyisha  watumishi wao kazi  katika mazingira magumu na hatarishi.

“Sasa natoa onyo kwa wamiliki na waajiri wa viwanda kuwa Viwanda tunavitaka ila tunahitaji staha kwa watumishi , hivyo basi tutachukua hatua kali kwa mmiliki yeyote atakaenda kinyume na hili hatutamvumilia kwa lolote “ alisema Mhandisi Ndikilo.

Nae kwa upande wake Mwenyekiti wa TUCTA Mkoa Pwani alisema kuwa vyama vya wafanyakazi vitaendelea kutumia njia ya majadiliano na Serikali katika kutatua au kumaliza matatizo yote yanayowakabili wafanyakazi.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.