• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

Wakazi Pwani wasaidieni watoto Yatima -RC Kunenge

Posted on: December 23rd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge ametoa wito kwa wakazi wa mkoa huo kufuata moyo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan wa kuwasaidia watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu na kwamba kufanya hivyo ni ibada.

Mhe. Kunenge ameyasema hayo leo Disemba 23, 2022 wakati akikabidhi msaada wa vyakula vilivyotolewa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa watoto yatima wanaolelewa kwenye kituo cha Madina, Vikawe Halmashauri ya Kibaha Mji Mkoani Pwani.

Vyakula vilivyokabidhiwa ni mchele, mbuzi wawili, maharage, viungo na mafuta.

Mhe. Kunenge amesema Dkt. Samia ni Rais wa nchi lakini hakuangalia nafasi ya madaraka aliyonayo na kuguswa kuwasaidia watoto yatima kwa kuwapatia msaada wa vyakula ili washiriki na watoto wengine duniani kusheherekea sikukuu ya Krismas na mwaka mpya.

"Nitoe wito kwa wakazi wa mkoa wa Pwani, watoto hawa ni wakwetu hivyo tunajukumu la kuwasaidia," alisema Mhe. Kunenge.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo, mlezi wa watoto katika kituo cha watoto yatima cha Madina Fatuma Salum, pamoja na watoto wanaolelewa katika kituo hicho wamemshukuru Rais Dkt. Samia kwa msaada huo na kwamba amewafanya kuwa wenye furaha kama ilivyo kwa watoto wenye wazazi.

kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM wilaya ya kibaha mwalimu mwajuma Nyamka aliyemwakilisha mwenyekiti wa CCM mkoa wa pwani Mwinshehe Mlao amesema licha ya kwamba rais Dkt. Samia amefanya ibada kwa kuwasaidia watoto yatima lakini pia ametekeleza ilani ya chama hicho iliyoanisha kuyasaidia makundi hayo.

Rais Dkt. Samia amekuwa akitoa msaada wa vyakula kwa watoto yatima na wanaolelewa katika vituo mbalimbali vilivyopo katika mikoa yote hapa nchini Kila mwaka hususani wakati wa sikukuu za kidini na za kufunga mwaka.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.

  • Situs Toto
  • Situs Slot Gacor
  • AXL777
  • Situs Toto
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • DORA77
  • DORA77
  • DORA77
  • Toto Togel
  • Situs Toto
  • AXL777
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Toto Slot Gacor
  • Toto Slot
  • Toto Slot
  • DORA77
  • KOI200
  • KOI200
  • SILVAWIN
  • AXL777
  • YAMITOTO
  • NABITOTO
  • YAMITOTO
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200