• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Wakazi wa Mwanalugali wapata Zahanati

Posted on: June 28th, 2022

WAkazi zaidi ya 3,500 wa Mitaa ya Mwanalugali A na B Kata ya Tumbi Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani, wanatarajia kuondokana na kero ya kutembea umbali wa kilometa 10 kufuata huduma za afya kituo cha afya Mkoani na hospital ya Rufaa ya Tumbi baada ya ujenzi wa Zahanati ya Mwanalugali kukamilika mwezi Septemba mwaka huu.

Hayo yamebainika wakati Mkuu wa MKOA wa Pwani Abubakar Kuenge alipotembelea mradi wa miundombinu ulioibuliwa na wananchi na kufadhiliwa na Mfuko wa Maendeleo ya jamii (TASAF) katika eneo hilo na kutoa agizo kwa mganga Mkuu wa mkoa kuhakikisha wanaandaa wataalamu na watendaji wa afya mapema ili mradi ukianza wawepo tayari kutoa huduma.

Katika ziara yake hiyo, RC Kunenge alitoa agizo la idara ya Afya kuhakikisha kuwa kunakuwepo vifaa tiba ili huduma zianze Mara moja baada ya ukamilishaji wa mradi huo.

Pia Kunenge alitoa agizo kwa mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha na wataalamu wake kupima na kuandaa mchoro na Hati kwa eneo hilo ili kuondoa changamoto za migogoro ya ardhi.

Pamoja na hayo, Mkuu huyo wa Mkoa ameitaka Mamlaka ya maji na usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) na Shirika la Umeme (TANESCO) kuweka Mazingira mazuri ya upatikanaji wa huduma hizo huku akiielekeza TARURA kuhakikisha inachonga barabara zote zinazoelekea katika Zahanati ya Mwanalugali ili kuondoa usumbufu.

Awali, mkazi wa Mwanalugali Frida Mvalla alisema mradi huo utakuwa mkombozi kwao kwani walikuwa wakipata shida hasa wajawazito na Watoto pamoja na kuhangaika endapo kunatokea wagonjwa nyakati za usiku.

Nae Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Mji wa Kibaha Anita Lioka alisema wananchi wameibua mradi huo na TASAF imefadhili na utagharimu kiasi cha sh. milioni 113.6. hadi kukamilika.

Wakazi wa eneo hilo pia wameomba kuongezwa jengo la kujifungulia ili kusaidia wakinamama na watoto.

Ujenzi huo ulioanza mwezi machi mwaka huu umefikia asilimia 70 ya utekelezaji.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.