• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Watendaji wa Vijiji na Mitaa Wapewa Mafunzo ya Mfumo wa iMES kwa Ajili ya Kukusanya Takwimu za Kijinsia Mkoani Pwani.

Posted on: October 3rd, 2025

Mafunzo ya matumizi ya Mfumo wa Integrated Monitoring and Evaluation System (iMES) yamefanyika mkoani Pwani kwa lengo la kuwawezesha Maafisa Watendaji wa Vijiji na Mitaa kukusanya taarifa mbalimbali zenye mlengo wa kijinsia. Mafunzo haya yamefanyika kupitia Mradi wa Women’s Leadership and Economic Rights Project (WLER) unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI na Shirika la Umoja wa Mataifa la Wanawake (UN Women).

Mafunzo hayo ya siku tano yamefanyika kuanzia Septemba 29 hadi Oktoba 3, 2025, katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Kibaha. Washiriki walitoka katika Halmashauri za Chalinze, Kisarawe na Manispaa ya Kibaha.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Pwani, Bi. Grace Tete, alisema lengo kuu ni kuwajengea uwezo Maafisa Watendaji wa Vijiji/Mitaa 32 katika ukusanyaji na uingizaji wa taarifa sahihi kwenye mfumo wa iMES ili kusaidia kupanga na kufuatilia utekelezaji wa shughuli za maendeleo zenye kuzingatia usawa wa kijinsia.

“Kupitia mfumo huu, taarifa zitapatikana kwa urahisi na kwa wakati, jambo litakalosaidia kupanga maendeleo yanayolenga wanawake, wasichana na watu wenye ulemavu kwa ufanisi zaidi,” alisema Tete.

Washiriki wa mafunzo hayo walijumuisha Maafisa TEHAMA mmoja kutoka kila Halmashauri, Maafisa Maendeleo ya Jamii watatu kutoka kila Halmashauri, Maafisa Maendeleo ya Kata kutoka maeneo ya utekelezaji wa mradi (Msoga, Ubena, Pangani, Mkuza, Kisarawe na Masaki), pamoja na Maafisa Watendaji wa Vijiji/Mitaa 32.

Mradi wa WLER, unaofadhiliwa na UN Women, ulianza kutekelezwa mwaka 2022/2023 katika kata tisa za Mkoa wa Pwani, kwa lengo la kuhakikisha wanawake na watu wenye ulemavu wanashiriki kikamilifu katika vyombo vya maamuzi na kupata fursa mbalimbali za kiuchumi.

Mafunzo hayo yalijumuisha vipindi vya nadharia darasani na mafunzo kwa vitendo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza ushiriki wa wanawake katika uongozi na kuboresha hali zao za kiuchumi.


Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Watendaji wa Vijiji na Mitaa Wapewa Mafunzo ya Mfumo wa iMES kwa Ajili ya Kukusanya Takwimu za Kijinsia Mkoani Pwani.

    October 03, 2025
  • RC Kunenge: Aagiza Mradi wa IPOSA ulete Matokeo yanayoonekana.

    October 02, 2025
  • Mkoa wa Pwani Waendelea Kung’ara katika Utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF).

    September 30, 2025
  • Rais Samia Aipongeza Pwani Kwa Kuibeba Vyema Ajenda ya Kitaifa ya Uwekezaji Katika Viwanda.

    September 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.