• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahali tulipo
    • Dira na Dhima
    • Mamlaka
    • Majukumu na Kazi
    • Waliowahi kuwa Mkuu wa Mkoa
    • Waliowahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Maji
      • Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • Sheria
  • Wilaya
    • Kibaha
      • Kuhusu kibaha
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Bagamoyo
      • Kuhusu bagamoyo
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mafia
      • Kuhusu Mafia
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kisarawe
      • Kuhusu Kisarawe
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Mkuranga
      • Kuhusu mkuranga
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Rufiji
      • Kuhusu Rufiji
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
    • Kibiti
      • Kuhusu Kibiti
      • Utawala
      • Ulinzi na Usalama
  • Halmashauri
    • H/M Kibaha
    • H/W Kibaha
    • H/W Kisarawe
    • H/W Mafia
    • H/W Mkuranga
    • H/W Rufiji
    • H/W Kibiti
    • H/W Chalinze
    • H/W Bagamoyo
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Ardhi
    • Bandari ya Nchi Kavu
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Makala
    • Sheria
    • Hotuba
    • Fomu
    • Mpango Mkakati wa Mkoa
    • Fursa za Uwekezaji
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Nafasi za Kazi

Wawezesheni Maafisa Michezo,utamaduni pamoja na walimu wa Michezo ili kuleta mabadilikokatika sekta ya Michezo-Samataba

Posted on: May 26th, 2018

“Uendeshaji wa michezo kama hii na mashindano kama haya kunahitaji uwekezaji mkubwa na changamoto za kibajeti ni nyingi , hata hivyo uwekezaji huu ni muhimu sana katika maendeleo ya Mkoa wetu  hivyo hatuna budi kuwekeza katika michezo ili kuwajengea vijana wetu misingi bora katika suala zima la michezo na hatuna budi kufanya hivyo ,na tunakila sababu kufanya hivyo.”

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala Mkoa Pwani ndugu Zuberi Samataba wakati akifungua mashindano ya UMISETA Mkoa Pwani katika viwanja vya shulerya Filbert Bayi vilivyopo mjini Kibaha.

Akifungua mashindano hayo Samataba aliwataka wanamichezo hao ambao ni wanafunzi wa shule za sekondari za Mkoa Pwani kuwa na nidhamu kwa kipindi chote cha mashindano hayo.

Katika kuendeleza suala zima la michezo Mkoa wa Pwani Katibu Tawala Samataba amezitaka  Halmashauri zote za Mkoa Pwani kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya uendeshaji wa michezo ili kuweza kusaidia  kuwa na timu bora ambayo itaweza kuleta matokeo mazuri katika michezo.

Samataba alisema kuwa “tukiwa na bajeti ya kutosha ya kuendesha michezo nina amini maandalizi na mashindano yatakuwa  mazuri katika ngazi ya Halmashauri na Mkoa.”

Aidha amewataka maafisa Michezo na Utamaduni na Walimu wa michezo kutumia vyema taaluma  zao katika kuendeleza michezo Mkoani Pwani. Hata hivyo aliwataka wakurugenzi wawawezeshe maafisa hao na walimu wa michezo katika kuendeleza taaluma zao ili waweze kuleta sifa kimkoa na Kitaifa kwa ujumla.

Katika hatua nyingine Samataba  alisema kuwa mkoa wa Pwani sasa upo katika utekelezaji wa sera  ya viwanda hivyo amewataka wanamichezo hao kuongeza juhudi katika michezo na taaluma nyingine ili kuweza kujipatia ajira mbalimbali katika viwanda hivyo.

Michezo ya umiseta Mkoa wa Pwani imeshirikisha Halmashauri zote za Mkoa Pwani na  imeanza rasmi tarehe 26 Mei 2018 na inatarajia kumalizika tarehe 28 Mei 2018 na imejumuisha michezo mbalimbali ikiwemo Mpira wa Miguu kwa  wavulana na wasichana,Mpira wa mikono kwa  Wavulana na wasichana,Mpira wa wavu wavulana na wasichana ,Mpira wa kikapu wavulana na wasichana ,mpira wa pete wasichana tu,Riadha wavulana na Wasichana , Sanaa za maigizo , Ngoma na Mashairi.

Matangazo

  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Baraza la Biashara Mkoa wa Pwani July 04, 2023
  • Uzinduzi wa Program Jumuishi ya Malezi , Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Mkoa wa Pwani October 04, 2023
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA PWANI, OKTOBA 11,2023 October 10, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RS Pwani Yaibuka Kidedea kwa Ushindi wa "-1 Dhidi ya Kibaha TC

    May 01, 2025
  • Rais Samia Apongezwa kwa kuwa Kiongozi wa Mfano katika Maadhimisho ya Mei Mosi Mkoani Pwani

    May 01, 2025
  • RC Kunenge Aagiza CORECU Kutekeleza Maomo ya Rais Samia Kuhusub Ushirika

    April 30, 2025
  • Spika Tulia Asisitiza Umuhimu wa Muungano katika kuimarisha Umoja na Amani

    April 25, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.